Sunday, November 6, 2016

MKWASA ATANGAZA KIKOSI KITAKACHOWAVAA ZIMBABWE,AWACHUNIA AKINA YONDANI,MAHADHI NA KASEKE.

Na.Alex Mathias,Dar es salaam.
Kuelekea pambano la mchezo wa kimataifa wa kirafiki kati ya Timu ya Tanzania (Taifa Stars) wanaotarajiwa kucheza na timu ya Taifa ya Zimbwabwe Kocha Mkuu wa Charles Boniface Mkwasa kwa jina la utani Master ametaja kikosi ambacho kinatarajia kuingia kambini Novemba 7,2016.
Mkwasa ametangaza majina hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari,amesema kuwa wataanza kambi hiyo kwa ajili ya mchezo wao na Zimbwabwe na wachezaji wote wataungana na wengine kuanzia Novemba 13 baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania kumalizika.

“Mchezo wetu tunatarajia kucheza ugenini mjini Harare Novemba 13 hivyo tunauchukulia umuhimu mkubwa kwetu kutokana kuwa kwenye kalenda ya FIFA na sisi tunataka kushinda kutokana na kushuka vibaya katika ubora wa viwango vya FIFA na kufika mpaka nafasi ya 147 kitu ambacho ni hatari kwetu”alisema Mkwasa Wachezaji wanaounda kikosi hicho ni pamoja na Magolikipa:Aish Manura Azam,Said Kipao JKT Ruvu na Deogratius Munishi
 Mabeki:Erasto Nyoni, David Mwantika wa Azam, Michael Aidan wa JKT Ruvu, Mwinyi Hajji, Vincent Andrew wa Yanga, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ wa Simba  na James Josephat wa Prisons.
Viungo:Himid Mao wa Azam , Mohammed ‘Mo’ Ibrahim, Jonas Mkude na Muzamil Yassin wa Simba , wakati viungo wa pembeni ni Abdulrahman Mussa wa Ruvu Shooting, Shizza Kichuya, Jamal Mnyate wa Simba  na Simon Msuva wa Yanga.
Watupia shavu: Ibrahim Hajib wa Simba , John Bocco wa Azam FC, Elius Maguli timu ya Oman anacheza , Thomas Ulimwengu aliyemaliza mkataba wake TP Mazembe ya DRC , Omar Mponda wa Ndanda  na Mbwana Samatta wa K.R.C Genk ya Ubelgiji

No comments: