Sunday, November 20, 2016

JUKWAA LA KATIBA TANZANIA WAIBUKA,WADAI HAKUNA KUINYOOSHA NCHI BILA KATIBA IMARA,SASA WAZINDUA HARAKATI ZA KUDAI KATIBA MPYA RASMI


Mratibu wa Jukwa la katiba Tanzania JUKATA Ndugu Hebron Mwakagenda Pamoja na Viongozi wengine wa mashirika yanayoshirikiana na Jukata wakionyesha Kitabu maalum ambacho kimezinduliwa Leo kwa ajili ya kuhamasisha Upatikanaji wa katiba moya baada ya mchakato huo kukwama kusikujulikana.Kitabu hicho kinaeleza Mwelekeo wa katiba Mpya Tanzania,Tulikotoka,Tulipo,na Tuendeko(Picha na Exaud Mtei wa Habari24 Blog)
Wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiweka wazi mbele ya wanahabari kuwa mchakato wa Katiba mpya itabidi usubiri ili apate nafasi ya kuinyoosha nchi kwanza,nao Jukwaa la katiba Tanzania JUKATA wameibuka na kusema kuwa njia pekee ya kuinyoosha nchi ni kuwa na katiba mpya na sio vinginevyo.

Kauli hiyo ya jukwaa la katiba imekuja huku kukiwa na sintofaamu kuhusu kupatikana ama kutokupatikana kwa katiba mpya mchakato ambao ulisimama na kupisha uchaguzi mkuu mwaka 2015 na kuacha katika hatua ya Katiba Pendekezwa.
Akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam Mratibu wa jukwaa la katiba Tanzania Ndugu Hebron Mwakagenda amesema kuwa wameshtushwa na kauli ya serikali ya Tano kuwa mchakato wa Katiba mpya sio kipaumbele cha serikali ilihali katika Ilani ya chama cha mapinduzi ndio Ilikuwa moja ya ahadi zao za kuhakikisha kuwa katiba hiyo inapatikana.


“Tunampongeza Rais wa Tanzania Mh Dkt Magufuli kwa juhudi kubwa anazozifanya kuirejesha nchi nmahala inapostahili na JUKATA tunaamini kuwa katiba ndiyo chombo pekee ambacho kitamsaidia Rais Kuirudisha nchi kwenye Mstari unaostahili,katiba pia itafanya Rais magufuli aache Kumbukumbu ya kudumu ndani ya mioyo ya vichwa vya watanzania kwa miaka mingi ijayo”amesema Mwakagenda ambaye ni mratibu wa JUKATA.
Mratibu wa JUKATA Ndugu Hebroni Mwakagenda akizungumza na wanahabari leo.
Aidha JUKATA wamesema kuwa Duniani kote katiba ndiyo waraka unaowezesha  wananchi kujitambua kama Taifa,pia katiba ni waraka wa kiutawala unaoelezea bayana mgawanyo,madaraka,na majukumu ya vyombo mbalimbali vya dola katika nchi hivyo katiba ndio waraka mama wa kisheria unaoongoza shughuli zote za nchi na ni chimbuko la kisheria zote katika nchi,Hivyo kauli kuwa huu ni muda wa kuinyoosha nchi bila kuwa na katiba imara ni jambo la kupingwa wanaitaka serikali kurejesha mchakato wa katiba mapema.
Pamoja na hayo Jukata kwa kuonyesha kuwa huu ndio muda muafaka wa Kurejesha mchakato wa katiba nchini wamezindua kitabu maalum ambacho kinawahamashisha wananchi kuelewa mchakato huo ulipofikia na nini kifanyike ili kuweza kuipata katiba mpya kwa sasa.

No comments: