Sunday, November 27, 2016

“Wanaofanyiwa Ukatili wa Jinsia wafike Polisi kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto” ASP Matarimbo

Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Polisi wa Kinondoni ASP Fatuma Matarimbo akitfundisha somo la Jinsia katika Warsha ya Mafunzo katika kuadhimisha siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia-Mtaa/ wa Udoe/Masjid Udoe, Kariakoo-Bilal Muslim Mission of Tanzania, leo Dar es salaam.

Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Polisi Kinondoni ASP Fatuma Mitarimbo ameitaka jamii ya Kitanzania kwenda katika Dawati la Jinsia na Watoto ili kupunguza matatizo mbalimbali yanayosababishwa na Ukatili wa Kijinsia.
“Jeshi la Polisi nchini lina vituo 417 vya Dawati la jinsia na Watoto Tanzania nzima, na watu wote wanakaribishwa katika vituo hivyo kuja kutoa taarifa ya matatizo yao ya Ukatili wa Kijinsia ili matatizo hayo tuweze kuyapunguza katika jamii yetu” amesema Mitarimbo.

ASP Mitarimbo amesema hayo leo katika Warsha ya mafuzo kwa Wajane, katika kuadhimisha siku ya 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia, katika Mtaa wa Udoe (Masjid Udoe), Bilal Muslim Mission of Tanzania, Kariakoo Dar es salaam.

Warsha hiyo iliandaliwa na Chama cha Wajane Tanzania / Tanzania Widows Association (TAWIA), ikishirikiana na WilDAF pamoja na Bilal Muslim Mission of Tanzania. ikiwa na Kauli mbiu"Funguka, pinga Ukatili wa Kijinsia, Elimu salama kwa wote"
Kuna aina kuu nne ya Ukatili wa jinsia ambayo ni Ukatili wa Mwili, ukatili wa Kisaikolojia, ukatili wa Kingono na ukatili wa Kiuchumi. “katili wa Kijinsia ni Kitendo chochote kinachoweza kumsababishia mtu mwingine kuwa na madhara, madhara hayo yanaweza kuwa madhara ya kimwili, kingono, kisaikolojia na Kiuchumi” amesema Mitarimbo

Aidha ASP Mitarmbo ametoa wito kwa Jamii kutoa taarifa katika Jeshi  Polisi kitengo cha Dawati la jinsia na Watoto, Misikitini, Makanisani, kwa Viongozi wa Dini na taasisi zinazohusika na kuzuia na kupambana na Ukatili wa Kijinsia ili kupunguza ukatili nchini" amesema ASP Mitarimbo

Chimbuko la kuadhimisha siku 16 ya kupinga ukatili wa kijinsia ni kutokana na mauaji ya kinyama kwa akina dada watatu ambao ni wa Kilamabela ambao walikuwa wanaishi katika nchi ya Dominika, waliuuwa mwaka 1960, chanzo cha kuuwawa kilisababishwa na Wanaume zao ambao walikuwa wanapinga uongozi wa mbaya wa kiongozi wao Leonard Tujilo.

Kwa upande wa Jeshi la Polisi Tanzania tangu mwaka 2009, Jeshi la Polisi liliona kwamba ukatili wa Kijinsia umeshika usikani/ unakuwa, ukatili wa kijinsia ukawa ni chanzo cha makosa, ni chanzo cha watoto wetu kuzagaa mitaani, ni chanzo cha ndoa nyingi kutengana/kuvunjika na ni chanzo kikubwa sana cha kupoteza baadhi ya vioungo.
Hapo jeshi la polisi likasema hapana, likawa linatafuta namna ya kupunguza vitendo kama hivi, kwani mara nyingi vitendo kama hivyo vinafanyika kwa siri,hivyo jeshi la polisi likaona umuhimu wa kufungua Dawati la jinsia na watoto ili kuwapa nafasi akina mama, baba na watoto kuja kulalamika na kutoa dukuduku lao na kunapolisi ambao wamefundishwa vizuri na hawawezi kuja kutoa siri.



Kulia ni Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Polisi wa Kinondoni ASP Fatuma Mitarimbo akimuelezea mambo ya Kijinsia Mkurugenzi wa Chama cha Wajane Tanzania / Tanzania Wisows Association (TAWIA) Madam Rose Sarwatt.

No comments: