Tuesday, December 27, 2016

MWALIMU ASHUSHIWA KIPIGO KWA KUMCHARANGA MAPANGA MWANAFUNZI WAKE SIKU YA KRISMASI

Kijana Limbe akipata matibabu
Mwalimu Pendo akipata matibabu
*****

MWANAFUNZI Marco Limbe(14) aliyemaliza darasa la saba mwaka huu katika shule ya msingi Yitwimila iliyoko kata ya Kiloleli wilaya ya Busega mkoani Simiyu amelazwa katika kituo cha afya Busega mara baada ya kuchalangwa mapanga kichwani na mdomoni na mwalimu wake.


Tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 11.30 jioni wakati mwanafunzi huyo alipokuwa akirejea nyumbani kwao akitokea katika malisho ya mifugo,alipokaribia katika shamba la mwalimu Pendo Gabriel ndipo mwalimu huyo alimkamata kijana huyo na kuanza kumcharanga kwa panga na kusababisha kijana Limbe kupoteza fahamu kwa muda wa masaa 6.

“Shuhuda wa tulio hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Manoga anasema ilikuwa kama mchezo lakini kumbe ni kweli kwani niliona mifugo ya Limbe iliyokuwa ikielekea nyumbani na huku Limbe akiwa nyuma ya mifugo hiyo katika barabara ambayo iko karibu na maeneo ya shule, ghafla nilimuona mwalimu Pendo wakishikana na kijana huyo na ndipo nikamuona akiwa na panga na kuanza kumcharanga”,alieleza.

"Nilikimbia katika tukio na kutoa msaada kwa wote lakini, watu walijaa na kuanza kumshambulia mwalimu Pendo kwa kumpiga ingawa jaribio hilo lilikwama baada ya mwenyekiti wa kijiji hicho Mshemas Bahai.

Mwandishi wa habari hizi alikwenda katika kituo cha afya cha Nyashimo na kujionea hali mbaya kwa kijana Limbe ambaye alikuwa amepoteza fahamu kwa muda wa masaa 6 bila kujitambua na huku akiwa anaongezewa drip na kwa pembeni mwalimu Pendo Gabriel naye akipata matibabu ya jeraha lake kichwani ambAlo alishambuliwa na wananchi na huku akiwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi.

Mwenyekiti wa Sogesca Bahai Mshemas alisema sikukuu Krismasi imekuwa ni mbaya katika kijiji chake baada ya wananchi wenye hasira kali kufanya shambulio la kumshambulia mwalimu Pendo kwa kosa la kumcharanga na panga mwanafunzi wake aliyekuwa akitokea kwenye malisho na kupita karibu na shamba lake la mahindi akitokea katika malisho.

Hata hivyo alisema alifanikiwa kuwatuliza wananchi wa kijiji chake na kuanza kufanya mikakati ya kuwapeleka kituo cha afya ili wapate huduma za matibabu.

Aliongeza kuwa walifika polisi na kuandikiwa barua ya kwenda kutibiwa wote wawili mwalimu pamoja na mwanafunzi.

Kwa upande wake kaimu mganga mfawidhi wa kituo hicho cha afya Dk. Ayubu Ismail alithibitisha kuwapokea kwa majeruhi hao na kudai kuwa kijana Limbe ndiye aliyekuwa na hali mbaya zaidi kuliko mwalimu Pendo.

Aliongeza kuwa kijana ameshonwa nyuzi 9 katika sehemu zake zote alizopatwa na majeraha na huku mwalimu  akishonwa nyuzi 6.

“Ni kweli Limbe alikuwa ametokwa na damu nyingi sana na hivyo kumpelekea kupoteza fahamu kwa muda wa masaa 6 lakini hali yake inaendelea vizuri alisema Dk. Ismail”.

Na Shushu Joel- Busega

No comments: