Tuesday, December 27, 2016

MWANA HABARI MPOKI BUKUKU AZIKWA MKOANI DODOMA,ANGALIA PICHA


Alice Mama wa Marehemu Mpoki Bukuku akisaidiwa kuweka shada la maua katika kaburi la mwanaye Mpoki Bukuku wakati wa mazishi hayo yaliyofanyika Msalato nje kidogo ya mji wa Dodoma Marehemu Mpoki alifariki wiki iliyopita jijini Dar es salaam kwa kugongwa na gari maeneo ya Mwenge.
Watoto wa Marehemu Mpoki Bukuku Junior akiongozana na wadogo zake wakiweka shada la maua katika kaburi la baba yao wakati wa mazishi yaliyofanyika Msalato nje kidogo ya mji wa Dodoma.
Junior akiwa ameshikilia msalaba kwa majonzi wakati wa mazishi ya baba yake.
Mke wa Marehemu Mpoki Bukuku Bi. Lilian na watoto wake wakiaga mwili wa marehemu Mpoki Bukuku.
Jeneza lenye Mwili wa marehemu Mpoki Bukuku likiteremshwa kaburini.
Mbunge wa Singida Mashariki Mh Lazaro Nyalandu akiweka udongo kwenye kaburi la marehemu Mpoki Bukuku.
Mke wa Marehemu Bi Lilian akiweka udongo kwenye kaburi la marehemu mumewe.
Viongozi wa Dini wakiwa katika ibada hiyo ya mazishi.
Ndugu na jamaa waombolezaji wakiomboleza kwa uchungu mkubwa.
Naibu Waziri Anthony Mavunde pamoja na mbunge wa Singida Mashariki Mh. Razalo Nyalandu wakiombea mwili wa marehemu Mpoki Bukuku.
Waombolezaji wakiaga mwili wa marehemu
Junior akiaga mwili wa baba yake Marehemu Mpoki Bukuku.
Mama wa Marehemu Mama Alice akiaga mwili wa mtoto wake mpendwa marehemu Mpoki Bukuku.
Waombolezaji wakiwa katika mstari wa kuaga mwili wa marehemu.
Naibu Waziri Anthony Mavunde pamoja na mbunge wa Singida Mashariki Mh. Razalo Nyalandu wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Mpoki Bukuku.
Naibu Waziri Anthony Mavunde akitoa salamu za pole kwa wafiwa.
Naibu Waziri Anthony Mavunde akisaini kitabu cha maombolezo.
Mpiga picha wa magazeti ya Serikali TSN Habari Leo na Daily News Bw. Mroki Mroki akitoa salamu za pole kwa wafiwa kwa niaba ya chama cha wapigapicha.
Bw. John Bukuku akitoa salamu za pole kwa wafiwa kwa niaba ya Wana mitandao
Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoani Dodoma Bw. Chidawali akitoa salamu zake kwa niaba ya wanahabari mkoani humo.
Mbunge wa Singida mjini Mh. Lazaro Nyalandu akitoa salam za pole kwa wafiwa.
Waombolezaji wakiwa katika mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Mpoki Bukuku.
PICHA ZOTE WA HISANI YA FULL SHANGWE BLOG

No comments: