Wednesday, January 18, 2017

POLISI FEKI WATATU WANASWA KILIMANJARO WAKIIBIA WANANCHI


Polisi mkoani Kilimanjaro kwa kushirikiana na raia wema imewatia mbaroni watu watatu wanaodaiwa kujifanya ni askari wa jeshi hilo na kuwaibia wananchi fedha na mali. 

Habari zilizopatikana jana zilisema kuwa katika upekuzi uliofanywa kwenye moja ya nyumba anayoishi mmoja wa watuhumiwa hao, kulikutwa kitambulisho cha mwalimu aliyewahi kuibiwa mamilioni ya fedha akitokea benki. 


Kwa mujibu wa habari hizo, kundi la watu hao limekuwa likiendesha vitendo vyake katika maeneo ya kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi na mitaa mbalimbali, hususan karibu na duka la Nakumatt. 


Vyanzo mbalimbali vimedokeza watuhumiwa hao huwakamata watu na kuwapekua kisha kuwatuhumu kuwa fedha walizonazo au simu vimeibwa sehemu na wao ni washukiwa wanaotafutwa. 


Kamanda wa Polisi Mkoa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa jana alithibitisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao juzi saa nane mchana katika eneo la Njoro Relini

No comments: