Thursday, February 9, 2017

Askofu Gwajima Alipuka Dar muda Huu,amaliza na kuelekea Polisi mchana huu

Gwajima:- 
Namuomba Rais ambadilishie Kazi Makonda, hii ya Ukuu wa Mkoa kutawala na kuongoza hata watu usiowapenda imemshinda. Sisemi amfukuze hapana nasema ambadilishie Kazi.

Gwajima : Makonda ana chuki na wivu na mimi

Gwajima : alikasirika hata niliposhuka na helkopta yangu siku ya mechi ya viongozi wa dini na wabunge dodoma.

Gwajima : nilichelewa kidogo nikaamua kupanda helkopta yangu mpaka uwanjani kabisa.

Gwajima : mimi nilicheza namba kumi Makonda namba tisa, jicho alilokuwa ananiangalia ni la chuki mpaka nikawa nashangaa.

Gwajima : hii hapa picha niko na Makonda, naibu spika na viongozi wengine tukichangia ujenzi wa taifa mbona hajanikamata hapa kama ninauza unga? .

Gwajima : Makonda alikuja kanisani kwangu na marehemu sitta na akapanda mazabauni je hakujua kama nauza unga? 

Gwajima : hili ni shambulio kwa kanisa sio kwa Gwajima

Gwajima : hili ni shambulio kwa wote walio okoka tuonekane hatufai

Gwajima : hili ni shambulio kwa maaskofu wote na wachungaji wote

Gwajima : kwa sababu Gwajima ana kanisa kubwa

Gwajima : kwa sababu Gwajima ana waumini zaidi ya elf sabini kanisani kwake na makanisa zaidi ya 400 nchi nzima.

Gwajima : nilikuwa mkali Sana kwa serikali ya awamu ya nne na kikwete

Gwajima : nilikemea sana kupotea kwa ndovu kila siku

Gwajima; Makonda anafanya hivi kwa maslahi ya Nani? .

Gwajima : Makonda anafanya hivi kufurahisha serikali iliyopita ionekana nimekomolewa.

Gwajima : Hili ni shambulio kwa Ukristo. Rais wangu mpendwa mbadilishie Kazi Makonda.

Gwajima : Makonda hajatumwa na Rais kufanya anayoyafanya

Gwajima : mimi namfahamu vizuri Rais, hawezi kumtuma Makonda kufanya hivi.

Gwajima : Makonda atavuka mipaka sasa, atakemea Polisi, atakemea jeshi, atakemea wabunge

Gwajima : Makonda atakemea mpaka waziri mkuu.

Gwajima; wenzetu wabunge wameungana kutumia sheria na kanuni zao watamuhoji.

Gwajima : sisi raia wa kawaida tusio na sheria wala kanuni za kututetea tutashtaki wapi? .

No comments: