Monday, February 20, 2017

WANACHAMA WA TANZANIA GIRL GUIDS WAFANYA USAFI MAGOMENI KOTA, COCO BEACH DAR

 Walimu na wanafunzi wa shule za Msimbazi na Mongo la ndege ambao ni wanachama wa chama cha Tanzania Girl Guids (TGGA), wakijitolea kufanya usafi katika viwanja vya Magomeni Kota, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya shamra shamra ya maadhimisho ya wiki ya utoaji huduma kwa wahitaji.


Wanachama hao walioongozwa na Mwenyeikiti wa chama hicho, Profesa Martha Qorro pamoja na Katibu wa Taifa wa TGGA, Grace Shaba walifanya usafi katika viwanja vya Magomeni Kota na Ufukwe wa Coco.



Walimu na wanafunzi kutoka shule za Mugabe, Urafiki, Mongo la Ndege na Msimbazi ambao ni wanachama wa TGGA walishiriki ipasavyo kwenye usafi huo.



Pia baadhi ya wanachama wa TGGA walikwenda kutoa msaada wa vitu mbalimbali katika Kituo cha Taifa cha Yatima cha Kurasini, Dar es Salaam.

 Wanafunzi wa Shule za Mugabe na Urafiki na walimu wao wakifanya usafi katika Ufukwe wa Coco Oysterbay, Dar es Salaam wakati wa kuadhimisha waiki hiyo ya utoaji huduma kwa wahitaji
 Wanachama wa TGGA wakifanya usafi katika viwanja vya Magomeni Kota
 Mwenyekiti wa TGGA, Profesa Martha Qorro (kushoto) na Juma Rashid wakiungana na wanachama wengine wa chama hicho kufanya usafi katika Ufukwe wa Coco, Oysterbay Dar es Salaam 
 Mwenyekiti wa TGGA, Profesa Martha Qorro (kushoto) na Juma Rashid wakiungana na wanachama wengine wa chama hicho kufanya usafi katika Ufukwe wa Coco, Oysterbay Dar es Salaam 
 Usafi ukiendelea katika viwanja vya Magomeni Kota. Katikati ni Raia wa Madagascar Andriambolamanana Vahatrimama ambaye yupo TGGA kujifunza utamaduni, maadili, mila za Tanzania pamoja na masuala ya uongozi



 Mwanachama wa Girl Guids kutoka Rwanda Michelline Uwiringiyimana (katikati), ambaye yupo nchi kwa ajili ya kujifunza utamaduni na maadi pamoja masuala ya uongozi, akishiriki kufanya usafi katika viwanja vya Magomeni Kota,
  Mwanachama wa Girl Guids kutoka Rwanda Michelline Uwiringiyimana (kulia), ambaye yupo nchi kwa ajili ya kujifunza utamaduni na maadi pamoja masuala ya uongozi, akishiriki kufanya usafi katika viwanja vya Magomeni Kota,
 Rehema (kulia) wa TGGA akiwa na wanafunzi wa shule ya sekondari Msimbazi wakifanya usafi Magomeni Kota
 Katibu wa Taifa wa TGGA, Grace Shaba akishiriki kufanya usafi katika viwanja vya Magomeni Kota, Dar es Salaam
  Katibu wa Taifa wa TGGA, Grace Shaba (kulia) akishiriki kufanya usafi katika viwanja vya Magomeni Kota, Dar es Salaam
 Wanafunzi wa shule za Mugabe na Urafiki wakishiriki kufanya usafi katika eneo la Coco
 Wanafunzi wa shule za Mugabe na Urafiki wakishiriki kufanya usafi katika eneo la Coco
 Wanafunzi wa shule za Mugabe na Urafiki wakishiriki kufanya usafi katika eneo la Coco


 Mwalimu wa shule ya Mugabe, Notceris Seus ambaye ni mwanachama wa TGGA akishiriki kufanya usafi katika ufukwe wa Coco,
 Mwalimu wa Shule ya Msingi Urafiki, Scolastica Mpunga akiungana na wanafunzi kufanya usafi katika ufukwe wa Coco

No comments: