Tuesday, April 4, 2017

JUKATA WAMTWISHA ZIGO LA KATIBA MPYA WAZIRI PALAMAGAMBA KABUDI

Mkurugenzi Mtendaji  wa JUKATA Bwana Hebron Mwakagenda Pamoja na wadau mbalimbali wa Katiba nchini Tanzania wakizngumza na wanahabari Leo Jijini Dar es Salaam.
 Ikiwa ni siku kadhaa Tangu Serikali kupitia kwa waziri Mpya wa Katiba na Sheria Mh Palamagamba Kabudi Kutoa tamko Mjini Dodoma juu ya nia ya serikali kutaka kurejesha mchakato wa katiba mpya ili kumalizia mchalato huo ambao ulisimama kwa muda,Hatimaye Jukwaa la Katiba nchoni Tanzania JUKATA wameibuka na kuitaka serikali kuhakikisha kuwa mchakato huo  unazingatia matakwa ya watanzania na uhalisia wa mchakato wenyewe.

Akizungumza na wanahabari Leo Jijini Dar es salaam Mkurugenzi Mtendaji  wa JUKATA Bwana Hebron Mwakagenda Pamoja na Pongezi kwa waziri huyo kuteuliwa kushika nafasi hiyo nyeti JUKATA wamesema kuwa wanaamini kuwa sasa ni wakati muafaka wa kurejesha mchakato wa katiba kwani Waziri huyo pamoja na kuwa ni gwiji na mtaalam wa sheria na mambo ya katiba lakini pia ameshiriki kikamilifu katika mchalato huo akiwa kama Kamishna wa Tume ya mabadiliko ya katiba iliyokuwa chini ya Jaji Joseph Warioba hivyo wanaamini atautendea haki mchakato huo.
Mwakagenda amesema kuwa wao kama JUKATA wamepokea kwa mtizamo chanya kauli ya serikali ya kutaka kuendeeleza mchakato huo wa katiba mpya kauli ambayo ilitolewa na Waziri Kabudi Juzi ijumaa mkoani Dodoma,jambo ambalo wao kama Jukata wanaeleza kuwa Pamoja na Kauli hiyo ya Kutia matumaini bado ipo haja ya kutoa Ufafanuzi Zaidi juu ya nia hii ya kurekebisha sheria zinazosimamia mchakato wa katiba mpya kwa kutambua kuwa mchakato huo ulisimama wenyewe kwa kukumbwa na changamoto mbalimbali zikiwemo za ukosefu wa Busara.

Aidha wamemtaka Waziri huyo kuhakikisha kuwa katika Bunge hili la mwaka 2017 anapeleka miswada ya marekebisho ya sheria zinazosimamia mchakato huo ikiwa ni pamoja na sheria ya kuanisha ni hatua gani za kupita ili kufikia kupata katiba Mpya.

Aidha wameeleza kasikitiko yao kwa serikali kutotenga Fedha tena kwa mwaka wa pili kwa ajili ya kukamilisha mchakato huo ambao uliingia katika sintofahamau mapema mwaka juzi na hatimaye kusimamishwa kwa ajili ya kupisha uchaguzi. 


No comments: