Wednesday, April 26, 2017

NAPE KAAMUA KUYASEMA HAYA LEO KUHUSU CCM NA MAGUFULI


Ikiwa leo Tanzania inatimiza miaka 53 toka Tanganyika na Zanzibar zilipoungana mwaka 1964 na kuunda nchi ya Tanzania Mbunge wa jimbo la Mtama, Mh Nape Nnauye amefunguka na kusema CCM ndiyo waasisi wa Muungano huo.

Mhe Nape Nnauye anakiri kuwa licha ya mapungufu ya hapa na pale katika chama chake hicho lakini bado kinabakia kuwa chama bora cha mfano barani Afrika, Nape Nnauye amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter 

"CCM bado ni Chama bora cha mfano kwa Afrika! Ni imara na kina historia ndefu, nzuri iliyotukuka sana! Ndio waasisi wa Muungano Wetu, tuudumishe" alisisitiza Nape Nnauye

No comments: