Tuesday, April 25, 2017

RAIS MSTAAFU KIKWETE ASHTUA WATU KWA KAULI YAKE HII HUKUSU ELIMU


Suala la elimu kwa wote bado ni changamoto kubwa hususani kwa nchi masikini na za kipato cha wastani, amesema Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais mstaafu wa Tanzania na mjumbe wa Kamisheni ya kimataifa kuhusu ufadhili wa fursa za elimu duniani.

Kikwete ambaye alikuwepo Washington D.C kwenye mkutano wa ufadhili wa elimu wa mkakati mpya uliozinduliwa mwaka jana kwa nchi za Afrika "The Pioneer country Initiative" baada ya kuzuru nchi 14 zilizo katika mradi huo wa awali.

Dkt. Kikwete amesema alichobaini kuna matatizo makubwa matatu kwenye nchi masikini na nchi za uchumi wa kati ambapo vijana wengi wanaostahili kuwepo mashuleni hawapo mashuleni, lakini la pili ni kwamba wanafunzi waliopo mashuleni wengi wao hawamalizi masomo yao na jambo la tatu watu wanaomaliza masomo yao hawapati elimu wanayostahili kuipata.

Mbali na hilo Dkt Kikwete ameongeza kuwa tume imependekeza nchi husika zinapaswa kufanya mageuzi katika mifumo yao ya elimu ili kuweza kupata matokeo chanya katika sekta hiyo ya Elimu katika nchini zinazoendelea.

Nchi hizo ni pamoja na Botswana, Chad, Congo Brazzaville, Cote d'voire, Ethiopia, Gabon, Ghana, Malawi, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Tanzania, Tunisia na Uganda.

No comments: