Friday, April 28, 2017

TUNATAMBUA MCHANGO WENU -SERIKALI

Serikali imewahakikisha watetezi wa haki za binadamu  nchini kuwa serikali inatambua mchango  walionao  katika kuhakakisha haki za binadamu  zinalindwa na kudumishwa nchini na kuwaahidi kuwa Serikali  itaendelea kushirikiana nao  na kuwawekea mazingira stahiki ya watetezi wa haki za binadamu  kuendelea kufanya kazi zao kwa utimilivu.
Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Waziri wa Katiba na Sheria Prof Palamagamba Kabudi  mjini Dar es salaam katika maadhimisho ya Nne ya watetezi wa haki za binadamu nchini kwa niaba ya Makamu wa Rais mhe. Samia Suluhu Hassan.
Katika maadhimisho hayo Prof Kabudi alizindua taarifa ya hali ya haki za binadamu  kwa mwaka 2016 ambayo iliandaliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania.
Maaadhimisho hayo yameandaliwa na mtandao wa watetezi wa haki za binadamu nchini na kuhudhuriwa na watetezi wa  haki za binadmu kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.  Pia yamehudhuriwa na wawakilishi  wa malozi na mashirika ya kimataifa, Wizara na taasisi za serikali
Maadhimisho hayo ya mwaka huu yalikuwa na kauli mbiu isemayo kuboresha ushirikiano na serikali


No comments: