Tuesday, April 11, 2017

ZITTO,BASHE,RIDHIWAN KIKWETE,AESHI,NA NKAMIA WAIRARUA SERIKALI BUNGENI

KAULI ZA WABUNGE WA CCM BUNGENI LEO 11/04/2017

Hivi Waziri wa Habari alikwenda kufanya nini katika Press ya Roma, mkiambiwa mlimteka mtakataa? Bora kusema ukweli kuliko kukaa kimya, najua mtasema kwa kuwa nilikosa uwaziri No!  - Juma Nkamia (CCM)

Mimi nimekamatwa na kuteswa na Usalama wa Taifa. Nimenyanyaswa sana nchi hii. Ikibidi mnifukuze CCM (machozi) - Hussein Bashe (CCM)

Hakuna sababu ya Mwigulu kuendelea kukaa kimya wakati wananchi wanaishi kwa wasiwasi juu ya usalama wao. Kutoa kauli  kunasaidia kutoa hofu.-- Ridhiwani Kikwete (CCM)

Mimi ni miongoni mwa wabunge niliotishwa na Mkuu wa mkoa wa Dar, na mpaka sasa mimi sikanyagi Dar licha ya kuimisi sana -Hillary Aeshi (CCM)

Zitto naye akasema Haya-

1. Ben sanane alitekwa Na usalama wa taifa
2. Waliovamia clouds Ni kikosi cha ulinzi wa rais - Na anaweza kuthibitisha
3. Aliyemtolea nape bastola Ni afisa wa usalama wa taifa - Na anaweza kuthibitisha. 

No comments: