Saturday, May 6, 2017

TUILINDE AMANI TULIYONAYO-SHEIKH JALALA

Kiongozi Mkuu wa kiroho wa waislam wa dhehebu la Shia ITHNASHERIYA Tanzania Sheikh Hemed Jalala akizngumza na wanahabari Nje ya semina hiyo kuhusu malengo yake.
Na Exaud Mtei

Vijana nchini Tanzania wametakiwa kutumia dini zao kama viungo vya kudumisha Amani,utulivu,na upendo  uliopo sasa badala ya kutumia dini zao kutengeneza migogoro na mifarakano katika jamii jambo ambalo lina madhara makubwa katika ustawi wa taifa kwa Ujumla,
Mmmoja ya watoa mada katika semina hiyo Dr Josephat Muhoza ambaye ni Mtaalamu wa Falsafa Kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salam akizungumza na Wanahabari  nje ya umbumbi wa Nkuruma ilikofanyika semina Hiyo.
Kauli hiyo imetolewa na Kiongozi Mkuu wa kiroho wa waislam wa dhehebu la Shia ITHNASHERIYA Tanzania Sheikh Hemed Jalala wakati wa semina maalum iliyofanyika chuo kikuu cha Dar es salaam Ukumbi wa Nkuruma yenye lengo la kujadili kwa pamoja namna ya kumuunganisha Mwanadamu na dini yake.na mwanadamu kutambua Tunu zilizopo katika dini yake.
Sheikh Jalala amesema kuwa  Dunia kwa sasa inakabiliwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe ambayo katika nchi nyingi dini imekuwa kichocheo kikubwa cha migogoro na migongano hiyo jambo ambalo amesema semina hiyo imeamua kuwakutanisha Vijana Pamoja na wataalam mbalimbali kuwakumbusha namna bora ya kuitumia dini yao kulinda Amani na kuepuka migogoro kama hiyo.

“Tanzania inasifa ya Amani, upendo, utulivu, kuheshimiana, kutokubaguana, hivyo vijana tunahitajika kuhakikisha kuwa tunaenzi Tunu hizi kwa hali na mali ili tuendelee kuwa na sifa ya kisiwa cha Amani duniani”alisema Kiongozi huyo wa Dhehebu la Shia nchini.
Washiriki wakichangua mada
Semina hiyo ilihudhuriwa pia na Wataalam mbalimbali akiwemo Mwanafalsafa wa chuo kikuu cha Dar es salaam Dr Josephat Muhoza ambaye kwa upande wake amewataka watanzania kutanguliza Ubinadamu mbele na kisha dini zao baadae kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wamejiepusha na migogoro kama inayoshughudiwa katika mataifa mengo duniani.




No comments: