Tuesday, May 30, 2017

WAANDISHI WA HABARI ZA KILIMO TANZANIA (TAJF) WAKUTANA MALAIKA BEACH RESORT JIJINI MWANZA KUPANGA MIKAKATI

 Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Kilimo Tanzania (TAJF), Gerald Kitabu (kulia), akizungumza na waandishi wa habari wanachama wa TAJF wakati wa kikao kilichofanyika Ufukwe wa Malaika Beach Resort jijini Mwanza jana kujadili masuala mbalimbali ya chama hicho.

 Katibu wa Chama hicho, Elias Msuya akizungumza katika kikao hicho. Kulia ni Mtunza Fedha wa chama hicho, Ellen Manyangu.
 Wanachama wakiwa kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.

Na Dotto Mwaibale, Mwanza

WAANDISHI wa Habari wanaounda Chama cha Waandishi wa Habari za Kilimo wamekutana Malaika Beach Resort jijini Mwanza kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali ya chama hicho.

Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika jana Mwenyekiti wa chama hicho, Gerald Kitabu pamoja na mambo mengine alihimiza wanachama ambao bado hawajatoa michango yao ya mwaka waitoe ili kutunisha mfuko wa chama hicho.

"Ni muhimu wanachama ambao bado hawajaotoa michango yao kuhakikisha wanaitoa kwa wakati" alisema Kitabu.

Katibu wa Chama hicho, Elias Msuya alisema chama hicho kipo katika mchakato wa kutengeneza vitambulisho kwa ajili ya wanachama na wakati wowote vitakapo kuwa tayari vitatolewa kwa wahusika.



No comments: