Sunday, June 18, 2017

E FM WAUNGANA NA DIAMOND TRUST BANK(DTB) KUTOA MISAADA KWA WATOTO WENYE VICHWA VIKUBWA NA MIGONGO WAZI


Wazazi kote nchini wametakiwa kuwaharakisha matibabu watoto wao endapo watagundua kuwa wana matatizo ya kichwa kikubwa au mgongo wazi. Hayo yameelezwa leo Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Tiba na Mifupa ya MOI Dr. Respicious Boniface alipokuwa akipokea misaada ya dawa toka Diamond Trust Bank wakishirikiana na E Fm Radio.
Mkurugenzi Mtendaji wa Diamond Trust Bank Tawi la Morroco Bi. Sheena Y. Sinare akitembelea hodi za Watoto wenye Vichwa vikubwa na migongo wazi kwenye Taasisi ya MOI Muhimbili jijini Dar es salaam
Akiongea na waandishi wa Habari Dr. Respecious Boniface alipenda kuwashukuru DTB na E FM na alipenda kuwaomba wazazi wamuwaishe mapema pindi wanapogundua kuwa mtoto anatatizo moja wapo kati ya hayo kwani ukiwahi mtoto anapona na hata matibabu yake yanakuwa  hayana usumbufu sana kama unapomchelewesha.

Pia aliongezea kwa kusema tatizo hili sio Tanzania peke yake bali ni dunia nzima na tathmini inaonyesha kila kwenye watoto 1000 wanaozaliwa Duniani wawili lazima watakuwa na tatizo hilo. Na miongoni mwao asilimia 70 ni wenye Vichwa vikubwa na asilimia zilizobaki 30 ni wa Mgongo wazi.
Mkurugenzi wa DTB Tawi la Morroco Sheena Y. Sinare akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dr. Respicious Boniface misaada ya Dawa iliyotolewa mapema leo Muhimbili jijini Dar es salaam
Na Dr. Respecious Boniface alipenda kuzishauri Taasisi mbalimbali, Idara za Serikali na watu binafsi kuweza kuiga mfano wa DTB na E fm kwa kuwa na utaratibu wa kujitolea misaada kwa magonjwa mbalimbali ambao hawana uwezo. “Na wapo wengi sio tu kitengo cha MOI bali hata magonjwa mengine kama kansa na magonjwa mengineyo”.Alisema


Lakini pia afsa habari wa Diamond Trust Bank(DTB) Mr.Baguma Ambary  alipenda kushuru wauguzi wa MOI  kwa mapokezi yao mazuri na kuwaomba waendelee na moyo wa kujitolea kwa wagonjwa hao kwani sote tunafahamu kazi ngumu waliyonayo. Na pia alipenda kushauri taasisi mbalimbali kuweza kujitolea kama wao na siyo kila ifikapo siku ya Mtoto wa Afrika wao kwenda kuwaona Yatima pekee waangalie na watoto wanaoteseka kwa magonjwa kama hayo.
Afisa mahusiano wa Efm Radio Jesca Mwanyika akikabidhi misaada kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moi Dr. Respecious Boniface mapema leo jijini Dar es salaam

Wafanyakazi wa Diamond Trust Bank pamoja na E fm wakiwa na watoto wao kwenye picha ya pamoja baada ya kukabidhi misaada 
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiendelea Kumuhoji Mkurugenzi wa MOI juu ya changamoto za watoto hao na Matumizi ya Misaada hiyo aliyopokea 

Afisa Habari wa Diamond Trust Bank Bw. Baguma Ambary akiongea na Waandishi wa Habari juu ya misaada waliyotoa mapema leo jijini Dar es salaam
Afisa Habari wa DTB kulia bw. Baguma Ambary  na kushoto ni mkurugenzi wa DTB Tawi la Morroco Bi. Sheena Y. Sinare wakishangaa kitu na kati ni Afisa Mahusiano wa Efm Radio Bi Jesca Mwanyika

No comments: