Sunday, June 4, 2017

LHRC WAHAMASISHA UTALII WA NDANI,WAIPA SOMO SERIKALI KUTUNZA MAZINGIRA


Ikiwa Dunia inaadhimisha siku ya Mazingira,Kituo cha sheria na Haki za Binadamu LHRC wamefanya Ziara katika Hifadhi ya Taifa ya Saadani ikiwa ni Hatua ya Kuunga mkono serikali katika hatua inazochukua katika kuhamasisha utalii wa ndani pamoja a kutunza Mazingira yetu.

Katika ziara hiyo ya LHRC waliitumia kutoa Tamko kuishauri serikali katika njia Bora ya kutunza Mazingira pamoja na Kuhamasiaha Utali wa ndani.

Akizungumza na Mtandao huu ulioambatana katika Ziara hiyo Mwanasheria kutoka LHRC  Pasience  Mlowe Pamoja na Kuipongeza Serikali kwa kutoa Ofa ya wananchi kuingia katika Mbuga zetu Bure kipindi hiki cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira amesema kuwa Ipo haja sasa kwa Serikali kutizama njia Bora zaidi ya kuvitangaza Vivutio vyetu kimataifa, ikiwa ni pamoja na kutumia Vyombo vya Habari vya kimataifa kutangaza lengo likiwa ni kuvutia watalii Zaidi.Aidha katika kuhakikisha kuwa Tunakuza Utalii LHRC wameshauri Pia Kuwepo kwa shirika la ndege la Tanzania Imara ambalo litakuwa lina safari nyingi za kimataifa ili kuweza kuhamasiaha watalii kufika kwa wingi nchini 
Aidha LHRC wameishauri Serikali kuhakikisha inaongea nguvu katika Utoaji wa elimu ya Utunzaji wa mazingira na uhifadhi wa Vivutio vyetu jambo litakalosaidia kuokoa mazingira na viumbe vyetu ambavyo Tumekuwa tukivipoteza siku Baada ya siku.
Fortunata Ntwele Kutoka LHRC Akieleza machache yaliyowapeleke katika Hifadhi hiyo ambapo amesema kuwa pamoja na kuwa LHRC wanaangalia haki za binadamu lakini mazingira ni swala muhimu sana kwa Binadamu hivyo ni lazima kuyatunza mazingira ili kuwa binadamu imara wenye afya njema.


Athmani Mmbae ambaye ni afisa utalii wa SAADANI akieleza machache kwa wanahabari baada ya kuwakaribisha wageni kutoka LHRC,ambapo amesema kuwa  kutokana na Tangazo la serikali la kuwaruhusu wananchi kuingia Bure kumekuwa na ongezeko kubwa la wananchi wanaokuja kwa makundi kutizama vivutio mbalimbali pamoja na changamoto ya Mvua inayoendelea kote nchini.
NAKUPA NAFASI YA KUTIZAMA PICHA MBALIMBALI ZA ZIARA HIYO----







No comments: