Monday, June 5, 2017

MISS UBUNGO MSTAAFU AUNGANA NA DIWANI WA PUGU KUADHMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Miss Ubungo mstaafu  2014 Diana Kato leo ameadhimisha siku ya mazingira Duniani kwa kupanda miti na kufanya usafi kwenye shule ya msingi Minazi Mirefu iliyopo kata ya Kipawa manispaa ya Ilala jijini Dar es salaam.
kwenye shughuli hiyo Diana Kato alimualika Diwani wa kata ya Pugu Ndugu Boniventure Mfuru na waliweze kushirikiana kwa pamoja kuifanya shughuli hiyo. lakini pia waliweza kupewa ushirikiano wa kutosha na Mwalim mkuu msaidizi msaidizi wa shule hiyo Bi. Juliana Msinzo ambaye walikuwa nae mwanzo mpaka mwisho wa shughuli hiyo. 

Diwani wa kata ya Pugu Mh. Boniventure Mfuru akifafanua jambo mbele ya wanafunzi wa shule ya msingi Minazi Mirefu ikiwa leo ni siku ya mazingira duniani (kulia) ni Miss Ubungo 2014 ambaye pia ni mdau wa mradi wa maji kwenye shule za msingi na(kushoto) ni Juliana Msinzo Mwalimu Mkuu msaidizi wa shule ya msingi Minazi Mirefu

Wanafunzi wa shule ya msingi Minazi Mirefu wakisikiliza kwa makini nasaha wanazopewa na viongozi wa mazingira na faida zake ikiwa leo ni siku ya mazingira duniani
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Minazi Mirefu wakigombania zana za kufanyia kazi ili waweze kujumuika na Miss Ubungo 2014 pamoja na Mh. Diwani wa kata ya pugu kufanya usafi kwenye eno la shule yao ikiwa leo ni siku ya Mazingira Duniani

Mwanafunzi wa shule ya msingi Minazi Mirefu Tausi Mohamed akipanda mti kwa niaba ya wanafunzi wenzake ikiwa leo ni siku ya Mazingira duniani wanafunzi hao wakihadhimisha siku hiyo kwa kupanda miti na kufanya usafi pamoja na miss ubungo 2014 Diana Kato pamoja na Diwani wa kata ya Pugu Bw. Boniventure Mfuru.

Mwanafunzi wa shule ya msingi Minazi Mirefu Craige Alfred akipanda mti kwenye shule yao mradi uliodhaminiwa na Miss Ubungo 2014 ambaye pia ni mdau  na mradi wa maji mashuleni (water project) Diana Kato 

Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya msingi Minazi Mirefu Bi. Juliana Msinzo  akipanda mti kwenye shule yake akiadhimisha siku ya Mazingira Duniani hii ikiwa ni kulinda na kutunza mazingira.

Diwani wa kata ya Pugu Ndugu Boniventure Mfuru akipanda mti kwenye shule ya msingi Minazi Mirefu hii ikiwa leo ni maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani


Miss Ubungo 2014 Diana Kato akimwagilia maji mti weke baada ya kupanda hii ikiwa ni kutunza mazingira kwa kuwa leo ni siku ya mazingira duniani

Miss Ubungo 2014 Diana Kato akiwa na Boniventure Mfuru ambaye ni Diwani wa kata Pugu  wakishirikiana na wanafunzi wa shule ya msingi Minazi Mirefu  kufanya usafi kwenye eneo la shule hiyo  ikiwa leo ni siku ya Mazingira Duniani.

Wanafunzi wa shule ya msingi Minazi Mirefu wakishirikiana na Miss Ubungo 2014 Diana Kato kufanya usafi kwenye eneo la shule hiyo leo ikiwa ni siku ya mazingira duniani

Miss ubungo 2014 Diana Kato akiwa kwenye picha ya pamoja na Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya msingi Minazi Mirefu Bi. Juliana Msinzo pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo.

Miss Ubungo 2014 Diana Kato akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule Msingi Minazi Mirefu baada ya kumaliza kufanya usafi kwenye eneo la shule hiyo.

No comments: