Wednesday, June 21, 2017

MUACHENI RAIS AFANYE KAZI-ADC WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI KWA KUPAMBANA NA WEZI,WAWATAKA WAPINZANI WATULIE WASIMPANGIE CHA KUFANYA.

Katibu Mkuu wa chama cha ALLIANCE FOR DEMOCRATIC CHANGE ADC Ndugu Doyo Hassan Doyo akizngumza na Mtandao huu maswala mbalimbali yanayoendelea nchini kwa sasa mara baada ya kumaliza shughuli maalum ya kupata Futari iliyaondaliwa na chama Hicho kamao makuu Jijini Dar es salaam
 Ikiwa ni siku kadhaa kupita Tangu Mkurugenzi wa kampuni ya VIP Engendering na mmiliki mwenza wa zamani wa IPTL James Rugemalira na Habinder Seth Sigh, Mwenyekiti mtendaji wa PAP ambao walitajwa  katika Kashfa ya Escrow Kufikishwa mahakamani kwa kesi ya uhujumu uchumi Tanzania kupitia Acount ya Escrow Hatimaye chama cha siasa cha Allience for democratic Change kimeibuka na kupongeza Juhudi za Rais Magufuli za kutetea Rasilimali za nchi huku wakiwataka watanzania kumuacha Rais afanye kazi yake kwani yeye ndiye anayejua anataka kutupeleka wapi.ANAANDIKA EXAUD MTEI----
Katibu Mkuu wa chama cha ALLIANCE FOR DEMOCRATIC CHANGE ADC Ndugu Doyo Hassan Doyo akiwashukuru  watanzania mbalimbali waliofika katika futari hiyo
Akizungumza na waumini mbalimbali wa kiislam na watanzania katika Futari maalum iliyoandaliwa na chama hicho Katika makao makuu yake yaliyoko Jijini Dar es salaam Katibu mkuu wa chama hicho Doyo hassan Doyo amesema kuwa kitendo cha Rais Magufuli kuonyesha dhahiri kuuchukia ufisadi na kupambana nao ni kitendo cha kupongezwa na kila mtanzania na sio cha kubezwa kwani wapo wengi walioshindwa japo kufikia hapo alipofika kwa sasa.
Naibu katibu mkuu U.P.D.P, Ndugu F,MUKUWA akisalimia baada ya kuwakilisha chama chake  katika shughuli hiyo
Amesema kuwa watanzania sasa wanastahili kumuombea Rais wao na kumuunga mkono katika vita hii kubwa na kuacha maneno ya kubeza kwani vita hiyo sio ya Rais mwenyewe bali ni ya watanzania wote dhidi ya rasilimali za nchi kwa ujumla.
Akizungumzia sakata hilo la Account ya Escrow ambalo mpaka sasa limeshaondoka na vigogo wawili waliotajwa katika maazimio ya bunge, amesema kuwa Kama Rais ameanza na hao hatuna budi kuamini kuwa Rais ana nia njema ya kuwakamata wale wote waliohusika na sio wakati wa kumpangia Rais nani wa kumkamata kwani wakati anaanza hakuna aliyempangia kuanza.

“Kuna watu hasa wapinzani ambao sjui hata wanaongea nini hasa,wapo wanaosema kuwa Rais aende mbali na hapo yani akamate na wale wengine,mimi nasema hivi hivi Rais akihama na kuingia katika sakata la Richmond na kuamua kuwakamata wale waliotajwa niambieni nani atapona hapa mjini,tuache kumpangia kazi,yeye ndiye anayejua anataka kutufikisha wapi”Amesema Doyo mbele ya wanahabari leo.

Aidha akielezea uwezo wa Serikali ya Tano katika kutatua changamoto za watanzania amesema kuwa pamoja na wapinzani kunyimwa fursa za kufanya siasa kinyume na katiba lakini Sasa Rais Magufuli ameanza kuonyesha kuwa anarudi kwenye mstaari baada ya kuanza kufuata maazimio mbalimbali yaliyowekwa na watanzania likiwemo la kuwakamata vigogo wa IPTL walioajwa katika sakata la ESCROW.

Shughuli hiyo ya futari maalum iliyoandaliwa na ADC imewakutanisha watanzania mbalimbali wakiwemo wawakilishi wa vyama vya siasa kama F.Mukuwa ambaye ni Naibu katibu mkuu U.P.D.P, na viongozi mbalimbali ambapo katibu mkuu Doyo amewashukuru sana kwa kufika na kuwatakia maandalizi mema ya sikukuu ijayo.

No comments: