Wednesday, June 14, 2017

PATA UNDANI WA NGOMA YA STERIO NA RICH MAVOKO MPE HABARI

msanii wa muziki wa Bongo Hip Hop Sterio ambaye alifanya ngoma kali ambazo zilitikisa Bongo kama Ntabaki juu, Usione hatari aliyo mshirikisha Ben Poul na jana aliachia wimbo mpya aliyomshirikisha Rich Mavoko unaoitwa Mpe Habari na nyingne nying.
alisema alitamani kufanya kazi na diamond lakini haikuweza kuwa rahisi lakini juzi kati diamond alihojiwa na kusema sterio ni miongoni mwa wasanii anaowakubali basi ilikuwa ni njia rahisi kwa sterio na walipokutana aliweza kuongea nae na chibu hakuwa na kinyongo aliweza kumpa nafasi.

Sterio alichoambiwa na Diamond Platnumz “Akaniuliza kwanini nipo kimya, Stereo social network zimekufanya nini mbona unaweza kufanya vitu vikubwa sana kupitia mitandao ya kijamii, kwanini unapenda kujificha. Mimi nakuambia una kitu kikubwa kitoe, nataka ufanye kazi kisingizio sio studio, Laizier huyo hapo, mimi nitamonitor mambo yote. Wewe unaflow kali lakini huna chorus kali, hapa ni nyumba ya machorus makali,” amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM na kuongeza.
“Siku nimepangiwa kurekodi tunanza kutengeneza beat na Laizier, Rich akaingia na vibe ikaongezeka mule ndani na beat ilikamilika ndani ya muda mfupi, baada ya kurekodi kuna kipande katika huu wimbo nilirudishwa, Chibu alitaka hivyo. So unarudi unafanya, na unaona nguvu ya pamoja na kila mtu amenipokea kama brother, sijajisikia ugeni ni kama nipo tu siku nyingi Wasafi,” amesema Stereo.

No comments: