Friday, June 23, 2017

WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO NA CHAMA CHA MAWAKALA WA FORODHA TANZANIA WAZINDUA RASMI KONGAMANO LA GLOBAL LOGISTICS SUMMIT –TANZANIA 2017


Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mwasiliano kwa kushirikiana na Chama cha Mawakala wa Forodha (TAFFA) wana furaha kuujulisha umma kwamba  kwa mara ya kwanza kabisa Tanzania itakuwa mwenyeji wa Kongamano la Global Logistics Summit 2017.  Kongamano hilo litafanyika kwenye Hoteli ya Ramada Resort Dar Es Salaam, tarehe 23 hadi 26 Agosti 2017.

Kongamano hili la kiulimwengu litakaribisha zaidi ya wageni 350 wakiwa mawakala wa kusafirisha mizigo, wajumbe wa kibiashara, washiriki wa kibiashara, maafisa wa serikali, mabalozi kutoka ukanda wa Afrika na Mashariki ya Kati, n.k. Zaidi ya nchi 32 toka ulimwengu mzima zinategemewa kuhudhuria na kushiriki mkutano huu toka dunia nzima.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Prof. Makame Mbarawa ameipongeza TAFFA kwa jitihada zake za kutengeneza ufahamu ambao ulihitajika kwa muda mrefu katika sekta ya uchukuzi ambayo ni muhimu katika taifa lolote sababu inawezesha usafirishaji wa watu na mizigo.

“Kuleta kongamano la GLS, 2017 mlangoni mwetu ni mafanikio makubwa na pia fursa nzuri ya biashara zetu hasa katika kipindi hiki ambacho serikali yetu inahamasisha ongezeko la biashara na katika bara la Afrika na kwingineko.” alisema Waziri.

Kongamano hili la siku nne limesifiwa kuwa tukio kubwa la kiuwekezaji katika bara la Afrika ambao litashuhudia washiriki wote wakuu wakikusanyika. 

“Mahusiano miongoni mwa waagizaji, wauzaji, wasafirishaji, mawakala wa kusafirisha na kutoa mizigo ambao ni wachache kati ya wengi ili kuleta mabadiliko na kuongeza shughuli za usafirishaji katika ya sekta ya majini Tanzania, hivyo kuisaidia nchi kupata hadhi yake kama kitovu cha bandari ki-kanda na hatimaye kukuza uchumi wa Tanzania.”

Kongamano hili pia litaiwezesha Tanzania kupata fursa ya kukuza uchumi wake kupitia sekta ya usafirishaji na usambazaji na baadhi ya maswala kama uboreshaji wa bandari na kuifanya iwe ya kisasa, kuongeza vyanzo vya mapato na changamoto zingine zitapewa kipaumbele kwenye majadiliano.


Rais wa FIATA, Mr. Stanley Lim na wageni wengine waandamizi kutoka FIATA na wawakilishi wa nchi mbalimbali watahudhuria na kuongoza programu ambayo itajielekeza katika kuongelea maswala ya uchukuzi na biashara katika ukanda wa Afrika na Mashariki ya kati. 
Kongamano hili linafanyika wakati ambao wafanyabiashara wa Kitanzania wanahitaji uelewa zaidi pamoja na maarifa kuhusu njia bora za utendaji kazi zinazotumika katika dunia hii ya kidijitali ambapo teknolojia inatawala. Kwa hakika kuna fursa nyingi za ukuzaji wa biashara Tanzania kwa maana ya usafirisaji na uhifadhi wa mizigo hasa katika nchi zisizo na bahari kama Burundi, DRC, Rwanda, Zambia, Malawi na Uganda zinaweza kutumia bandari ya Dar es Salaam kama njia ya usafirishaji mizigo.

“Sisi kama TAFFA tunapiga hatua kuhakikisha tunaziwezesha biashara kupitia kongamano hili la GLS ambapo wadau mashuhuri na waliobobea katika fani hizi watatoa maarifa  bora kwa wasafirishaji wa kimataifa.  Hii ni mara ya kwanza kwa sisi kuwa wenyeji wa mkutano huu wa kiulimwengu. Tunafurahia sana kupata fursa hii ambayo itaitangaza Tanzania kama kituo kizuri cha usafirishaji.” Alielezea Ngatunga.

“Hii ni fursa muhimu kwa taasisi yoyote yenye maslahi na sekta ya usafirishaji iwe kama, wakala, kampuni ya bima, mtoa huduma, mwanasheria, mtoa bidhaa ama afisa biashara kutengeneza wigo na mahusiano ya kibiashara. Tunataka kuionyesha dunia kupitia mkutano huu kwamba Tanzania ni sehemu sahihi kwa biashara za ukanda huu.

Maudhui ya kongamano ni, “Kuimarisha Usafirishaji kwa ajili ya Uchumi endelevu.”

Kwa sekta ya utalii, kupitia wavuti ya kongamano http://globallogisticssummit.or.tz/ tumetangaza sehemu nyingi za vivutio vya Kitalii viliyopo Tanzania. Ni tegemeo letu kwamba wageni watakuwa na nusu siku ya kutembelea vivutio hivi kwenye siku ya nne na ya mwisho ya mkutano huu. Washiriki pia wameonyesha nia ya kutaka kutembelea mbuga ya Serengeti, Selous, Zanzibar na Mlima Kilimanjaro. Hii inaonyesha kwamba ingawa lengo kuu la mkutano ni sekta ya usafirishaji lakini pia kutakuwa na faida nyingi zitakazopatikana kwenye sekta ya utalii.

 





No comments: