Wednesday, July 12, 2017

Picha & Video: JINSI ROONEY ALIVYOTUA TANZANIA NA KIKOSI KIZIMA CHA EVERTON

Klabu ya Everton tayari imewasili Jijini Dar es Salam dakika chache zilizopita ikiwa inatokea nchini Uingereza huku ikiwakosa wachezaji wake watatu muhimu katika kikosi hicho kutokana na majeruhi waliyokuwa nayo.


Pamoja na hayo, timu ya Everton imeongozwa na mchezaji nyota Wayne Rooney pamoja na Davy Klaassen na Michael Keane ambao pia wamejiunga na klabu hivi karibuni.


Kikosi kamili cha Everton kilichotua leo ni Maarten Stekelenburg, Mateusz Hewelt, Chris Renshaw, Tom Davies, Phil Jagielka, Ashley Williams, Callum Connolly, Jonjoe Kenny, Michael Keane, Muhamed Besic, Leighton Baines, Morgan Schneiderlin, James McCarthy, Davy Klaassen.


Wengine ni Gareth Barry, Idrissa Gana Gueye, Joe Williams, Kieran Dowell, Kevin Mirallas, Wayne Rooney, Aaron Lennon, Dominic Calvert-Lewin, Ademola Lookman, Matthew Pennington, Yannick Bolasie.


Everton imewasili Tanzania kwaajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Gor Mahia ya nchini Kenya mchezo unaotarajiwa kuchezwa katika dimba la Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam siku ya Alhamisi ya wiki hii.

Kivutio kikubwa katika mapokezi ya timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya Uingereza ni wananchi wengi waliojitokeza kumshabikia Wayne Rooney.




ANGALIA VIDEO HAPA

No comments: