Tuesday, July 4, 2017

PROF. LIPUMBA AMJIBU MAALIM SEIF KUHUSU BODI YA WADHAMINI


Wiki iliyopita katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif alitoa tuhuma akidai kuwa RITA imesajili bodi ya wadhamini feki hivyo akatangaza kuwa atawashtaki, sasa leo Mwenyekiti wa chama hicho Lipumba amejibu kuhusu tuhuma alizozitoa Maalim Seif
“CUF bodi yake ilikuwa imeisha muda wake, wajumbe wa bodi mpya wamekubaliwa na kusajiliwa na RITA kwa taratibu za CUF, CUF hatukuwa na chombo cha kuweza kupeleka kesi mahakamani kwa mujibu wa taratibu za CUF, Bodi ya wadhamini ndio ina uwezo wa kupeleka kesi mahakamani kwa niaba ya Chama, hakuna mwingine anayeruhusiwa“-Prof Lipumba

No comments: