Monday, July 3, 2017

TIB GROUP KATIKA MAONYESHO YA SABA SABA 2017


TIB Group ina mashirika matatu yaliyoundwa kimkakati ili kuiwezesha serikali katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya nchi. Mashirika hayo ni

1.      TIB Development Bank Limited
2.      TIB Corporate Bank Limited
3.      TIB Rasilimali Limited

Pamoja na umoja huu, mashirika haya yanajitegemea kiundeshaji na utendaji,  kila moja likisimamiwa na kuongozwa na dira na dhamira yake chini ya uongozi na bodi zao nazote zikiwa chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.

TIB Group  tunakukaribisha  kutembelea banda letu la sabasaba ili upate elimu na taarifa mbali mbali kuhusu huduma zetu.

Taasisi zetu zinatoa huduma mbalimbali za kifedha ikiwamo  ushauri  katika masuala ya mitaji na uwekezaji, mikopo ya miradi ya kimaendeleo na miundo mbinu pamoja na huduma mbalimbali za kibenki za biashara.

UWEZO TUNAO......Tumejipanga kutoa huduma mbali mbali za kifedha ili kusaidia ukuwaji wa biashara katika kuwezesha maendeleo ya viwanda.




Mkurugeni  mtendaji wa  kampuni ya Global Packaging Ndg Joseph Wasonga(wa pili kulia) akiwapa maelezo wakurugenzi wa TIB juu ya bidhaa zinazotengenezwa na kampuni hiyo. Wa kwanza kushoto ndugu  Frank Nyabundege Mkurugenzi mkuu wa  wa TIB Corporate Bank . Wa pili kushoto Charles Singili –Mkurugenzi Mkuu wa TIB Development Bank na wa mwisho kulia ni Bi Theresia Soka mkuu wa kitengo cha masoko – TIB Corporate Bank Ltd. Kiwanda cha Global Packaging ni miongoni mwa wateja ambao wamenufaika na mikopo inayotolewa na benki ya TIB. Kiwanda hiki ni miongoni mwa viwanda vya kisasa ambavyo vinazalisha vifungashio mbali mbali.

TIB Development Bank Ltd (TIB DFI) ni Benki ya maendeleo inayojihusisha  na  kutoa mikopo mbali mbali ya muda wa kati na muda mrefu. Mikopo hii inalenga sekta muhimu zinazochochea   maendeleo ya nchi. Sekta hizo ni pamoja na  miundo mbinu, uanzishwaji na uundwaji wa viwanda mbalimbali, miradi ya Gesi, ufuaji wa madini, miradi ya kuongeza thamani katika mazao ya kilimo na miradi ya huduma za kijamii.
Uzoefu wa benki hii katika kuwezesha maeneo haya una msingi imara kutoka kuanzishwa kwa Taasisi hii mwaka 1970.
Kwa mawasiliano zaidi:www.tib.co.tz

Wafanyakazi wa TIB Group (TIB Development Bank Ltd, TIB Corporate Bank na TIB Rasilimali Ltd) wakiwa tayari kutoa huduma kwenye  viwanja vya Maonyesho  - Saba Saba.
TIB Corporate Bank Ltd (TIB CBL) ni benki ya  biashara inayomilikiwa na Serikali kwa 100%. Benki inatoa huduma zote za kibenki za kibishara kwa  mashirika na taasisi za aina mbalimbali za serikali na  binafsi , pia benki inatoa huduma kwa watu binafsi.
Benki ina matawi  6 kwa sasa,  Dar es salaam (3), Mwanza , Arusha na Mbeya.

Benki inatoa huduma mbalimbali  kutokana na mahitaji ya mteja. Baadhi ya  huduma hizo ni pamoja na; akaunti za aina mbalimbali kwa makampuni na watu binafsi, mikopo ya aina mbali mbali ya muda mfupi na wa kati, Dhamana za Kibenki(Guarantees),Uuzaji na ununuaji wa fedha za kigeni, ushauri wa uwezekaji katika hati fungani,ukusanyaji wa fedha na kuwezesha malipo ya jumla kwa makampuni pamoja na ulipaji wa mishahara kwa njia rahisi na ya haraka

Huduma zote hizi hutolewa kwa umahiri na ufanisi mkubwa ili kuhakikisha mteja anafurahia mahusiano yake na benki. Pia huduma ya ‘Premier Banking’ kwa wale wateja wanaopenda huduma maalumu na kujitofautisha zaidi. Kwa mawasiliano zaidi:www.tib.co.tz

Wafanya kazi wa TIB Corporate Bank Ltd katika picha ya pamoja, wakiwa  taya ri kuwahudumia wananchi mbalimbali watakao tembelea banda lao katika maonyesho hayo
TIB Rasilimali Ltd ni taasisi ya tatu katika muundo huu wa TIB Group inayojihusisha na masuala ya uwekezaji katika masoko ya mitaji kama vile ununuaji na uuzaji wa hisa za makampuni yaliyoorodheshwa kwenye soko la hisa Dar es salaam (DSE). Pia kutoa ushauri wa kifedha na kuwezesha utafutaji wa mitaji.

TIB Rasilimali ndio wakala pekee wa soko la hisa la Dar Es salaam inayomilikiwa na serikali. Imesajiliwa na mamlaka ya masoko ya mitaji na dhamana(CMSA),pia inajihusisha na masuala ya usimamizi wa fedha (fund management) chini ya usajili wa Mamlaka ya usimamizi wa mifuko ya jamii (SSRA).Kwa mawasiliano zaidi:invest@rasilimali.tib.co.tz 


No comments: