Tuesday, October 10, 2017

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA KUPINGA ADHABU YA KIFO DUNIANI LHRC IMETOA MAPENDEKEZO HAYA KWA SERIKALI YA TANZANIA

Ikiwa leo ni siku ya maadhimisho ya kupinga adhabu ya kifo duniani kituo cha sharia na haki za binadamu LHRC kikiungana na mtandao wa kupinga adhabu ya kifo duniani kuadhimisha maadhimisho ya 15 ya kupinga adhabu hiyo.
Image result for adhabu ya kifo tanzania
Akiongea na waandishi wa habari mapema leo jijini dar es salaam kaimu mkurugenzi wa kituo hicho Bi. Anna Henga alisema kituo chao kitaendelea kupinga adhabu hiyo mpaka itakapoondolewa katika sharia ya Tanzania hii ikiwa ni kulinda na kuheshimu haki za binadamu ikiwemo haki ya msingi ya kuishi.

Anna Henga aliendelea kwa kusema adhabu ya kifo ni adahabu ya kikatili inayokinzana na misingi utu na haki za binadamu hivyo haifai kuwepo kwa nchi kama Tanzania ambayo imeingia na kusaini mikataba ya kimataifa na ya kikanda ya kutetea na kulinda na kuheshimu haki za binadamu.

Ingawa inafahamika kuwa adhabu ya kifo utolewa kwa makosa kama kuua kwa kukusudia, makosa ya uhaini pamoja na ugaidi, na hili siyo kwa mikataba ya kimataifa pekee bali hata katiba ya nchi ibala ya 14 inalinda uhuru na haki ya kuishi.
Kaimu mkurugenzi huyo aliendelea kwa kusema kuwa kwa mujibu wa ripoti ya haki za binadamu ya mwaka 2015 ilionyesha kuwa watu 472 walihukumiwa adhabu hiyo ya kunyongwa na kati ya hao 452 ni wananume na 20 pekee ni wanawake, na kati ya hao 228 wanasubiri kunyongwa na 244 wanasubiri rufaa za ingawa adhabu hiyo haijatekelezwa toka mwaka 1994 japo kuwa mahakama inaendelea kutoa adhabu hiyo.

Lakini pia imeonekana kuwa adhabu hii inawakumba sana wale watu masikini wasioweza kuwa na uwakilishi wa kisheria na wanyonge na pia ni vigumu pia kuthibitisha kweli huyu aliyeshikwa ni mtuhumiwa kweli aliyetenda kosa ni vigumu kupata ushahidi wa moja kwa moja.

Na jambo lingine adhabu hii haimpi nafasi mtuhumiwa ya kujirekebisha na badala yake inakuwa ni ya kulipiza kisasi na hakuna ushahidi wowote wa kuthibitisha kama kupitia adhabu hii kuna watu wamejifunza na badala yake mauaji yanazidi kuendelea.
Baada ya hayo yote serikali imetakiwa kuyafanya yafuatayo ikiwa ni mapendekezo ya kituo hicho.

Serikali inatakiwa kurekebisha kanuni ya adhabu ya sharia ya ugaidi yenye kutoa adhabu ya kifo kwa kosa la mauaji, uhaini na ugaidi.

Serikali kuwaelimisha wananchi kuhusu kuheshimu haki za binadamu hususani haki ya kuishi na kuweka mazingira ya uheshimuji wa haki hiyo.

Serikali kubadilisha adhabu ya kifo na kuweka adhabu mbadala kwa wafungwa waliopo magerezani sasa kama kuwapa adhabu ya muda mrefu gerezani nk.
Kwa kuwa imeonekana adhabu hii imekuwa ikimkera rais basi yeye anatakiwa kuwa kinara wa kuitisha mkutano wa kuiondoa adhabu hii ili yeye na majaji waondokane na mzigo huu mkubwa wa kutwaa roho za watu.


No comments: