Tuesday, October 10, 2017

WAPENZI WA BONGO MOVIE FILAMU KALI YA MAMUU KUZINDULIWA HIVI KARIBUNI KING D HOTEL

MSANII wafilamu na tasnia ya tamthiliya nchini Rakheem David amepanga kuwapa raha mashabiki wake katika uzinduzi wa ujio mpya wa filamu iitwayo 'Mammu'.
Akiongea na habari 24 jijini Dar es Salaam jana alisema kuwa uzinduzi huo utafanyika King D Hotel iliyopo Sinza maeneo ya Afrikasana. 

"Katika uzinduzi wangu nimejipanga kwa watakao fika watapita kwenye Red Carpet sambamba na kufanya mahojiano, "alisema Rakheem. 

Rakheem alisema mara baada ya kua nimekamilisha uchukuaji wa picha katika filamu yangu kuwa kamili kuingia sokoni, kampuni ya  Afrocinema Tours  Campany chini ya Richard Kabisi ndio iliyoongea nami kuhusu kufanya uzinduzi na nitaanza kuisambaza filamu yangu mwenyewe  mara baada ya uzinduzi.
                                 
Aidha Nyota huyo ambaye tayari ni mwenye umaarufu, awali amewahi kufanya vema katika filamu kama iliyoitwa 'Kibajaj iliyoshirikisha nyota wengine kama Mboto, Irene Poul pamoja na nyingine iliyoitwa 'Mama Ntilie 'iliyoshirikisha nyota kama Gabon, King Majuto pamoja na Irene Poul. 

Rakheem ameweza kufanya kweli pia kupitia tamthiliya ya Duty inayooneshwa kupitia Star Tv kila siku za jumatano saa 1:00 usiku. 

No comments: