Thursday, November 23, 2017

WANAHARAKATI WA GDSS KUPEWA ELIMU KUHUSU MAMBO YA MSINGI YA KUFANYA ILI KUWA WAJASIRIAMALI KAMILI.

Wajasiriamali wa kote nchini wametakiwa kuwa na tabia ya kujiamini na kuwa wabunifu katika biashara zao kwani hii ni njia pekee itakayowatofautisha wao na wafanya biashara wengine.
Muwezeshaji Mariam Tambwe akitoa ufafanuzi wa jambo fulani, mapema jana katika Semina ya ujasiriamali iliyoandaliwa na TGNP Mtandao ofisini kwao Mabibo jijini Dar es salaam.
Hayo yamesemwa mapema jana na Muwezeshaji Mariam Tambwe ambaye pia ni mwalimu wa chuo cha biashara CBE alipokuwa akiendesha semina ya namna ya kubuni biashara kama mjasiriamali na kuifanya ikastawi na kuwa bora zaidi.

Akitoa elimu hiyo kwa washiriki wa GDSS alisema kuwa ili uwe mjasiriamali ni lazima uwe na vitu vikubwa vitatu vitakavyokufanya uweze kusonga mbele katika gurudumu la maendeleo ya biashara yako ambavyo ni Elimu, Ujuzi na Hulka.

Aliendelea kwa kusema kuwa si lazima kuwa na sifa zote tatu lakini walau uwe nazo hata mbili ili ujiite mjasiriamali na uweze kuzimudu changamoto zinazopatikana katika fani hiyo na si vinginevyo.

Lakini pia alisema kuwa kunachangamoto mbalimbali zinazowakabili wajasiriamali mbalimbali hasa wanawake, ikiwemo rushwa ya ngono kwa wateja wao au watu mbalimbali waliowazunguka katika maeneo yao ya biashara kwa kuwataka kimapenzi ili biashara zao ziweze kwenda vizuri.
Baadhi ya Wanaharakati wakifuatili kwa umakini Semina iliyofanyika mapema jana makao makuu ya Mtandao wa Jinsia  TGNP.
Na changamoto nyingine ni kwa wanawake kuwa na majukumu mengi ya kifamilia yanayowakabiri ikiwemo ulezi wa familia, kushughulikia wagonjwa na kuhakikisha watoto wanakuwa salama katika malezi na hata kiafya bora.

Muwezeshaji huyo aliendelea kusema kuwa changamoto nyingine kubwa ni kwa wanawake baadhi ya maeneo hawapewi nafasi ya kumiliki ardhi wakati kwa ulimwengu wa sasa unapohitaji mkopo wa kujiendeleza katika biashara ni lazima uwe na kitu cha kuweka rehani ambacho ni mali isiyohamishika kama ardhi.

Aidha Dada Mariam  alisema ili uwe mjasiriamali mzuri ni vema uwe unazaliasha ama kuagiza bidhaa nyingi isije kutokea mteja akaja na akakosa bidhaa, kwani akikosa zaidi ya mara mbili anaacha kuja kwako na kwenda sehemu nyingine na unakuwa umempoteza wateja.

Lakini pia mjasiriamali anatakiwa kuwa na utofauti wa bidhaa zake na hii sio kwa kuwa na kitu ambacho hakijawahi kutokea ama kuonekana sehemu hiyo, ila awe na kitu chenye utofauti na ubora zaidi ya wengine.
Baadhi ya washiriki wa semina za Jinsia na Maendeleo GDSS  wakimsikiliza kwa umakini Muwezeshaji wa semina hiyo Dada Mariam Tambwe akiwaelezea namna ya kufanya ili wawe Wajasiliamali kamili.

No comments: