Thursday, November 23, 2017

MATAWI YA EXIM BENKI YAPATA UTHIBITISHO WA KIMATAIFA SOMA HAPA KIJUA ZAIDI

Leo ikiwa ni tarehe 23 ya mwezi novemba benki ya Exim Tanzania imekuwa ya kwanza nchini kwa matawi yake kupata cheti cha ISO 9001:2015 ikiwa kama uthibitisho wa ubora wa kimataifa kutoka shirika la viwango la kimataifa.
Mkuu wa Rasilimali watu wa Exim Benki Bw.Fredreick Kanga akitoa ufafanuzi wa jambo fulani mbele ya waandishi wa habari ambao hawapo pichani, mapema leo makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es salaam
Ikiwa ni jukumu lao ISO kuzingatia kanuni na ubora wa viwango wa kimataifa ikiwemo katika kujikita katika kuboresha huduma kwa wateja, kuangalia hamasa na msukumo wa viongozi wa juu mashirika, michakato na oparesheni zinavyoendeshwa, Exim benki imeonekana kuwa na vigezo hivyo na kutunukiwa cheti na ISO.

Akiongea na waandishi wa habari katika hafla ya kupokea cheti hicho Mkuu wa Rasilimali watu Bwa. Fredreik kanga alisema uthibitisho huo ni miongoni mwa mafanikio makubwa ambayo benki hiyo imepata ikiwa ni pamoja na benki kupata tuzo hivi karibuni kutoka banker – Afrika Mashariki kuwa benki bora kwa wateja binafsi.

“Kupata uthibitisho huu kutoka ISO ni hatua muhimu katika kuonyesha msimamo wetu wa kutoa huduma bora zaidi kwa wateja wetu, lengo letu ni kuendelea kuboresha imani katika soko kwa wateja wetu, kuboresha utoaji huduma, kupunguza muda wa kutoa huduma, kuwa tofauti na benki zingine, kuongeza ufanisi na pia kupata faida na kuongeza soko letu” alisema Frederick Kanga

Mradi huo ulichukua takribani miezi 6, ulianza kwa kutoa mafunzo kwa wafanyakazi juu ya kanuni za usimamizi wa ubora wa kimataifa ISO 2001:2015, pia uboreshwaji wa viwango, ukaguzi wa ndani utengenezaji wa ratiba ya matukio kuwekamipango muhimu hadi kufikia upatikanaji wa uthibitisho huo na ilikuwa kujitoa kwao na utendaji bora ambao umesababisha tuzo hii.
Katika kuhakikisha inajenga chapa bora benki ya Exim imejikita katika kuhakikisha inakuwa na bidhaa za kivumbuzi , mahusiano bora na kutoa huduma kwa haraka, na ikumbukwe kuwa mchakato huu wa kupata cheti cha ISO ulianza mwaka huu na Clock Tower na Namanga yaliteuliwa kuwa ya kwanza kupatiwa mchakato huo.

Mkuu wa rasilimali watu wa Exim aliendelea kwa kusema “Tukiwa kama benki yenye uthibitisho wa ISO tutahakikisha utoaji wa huduma na bidhaa ni bora, ufanisi katika operesheni na mawasiliano, hamasa kwa wafanya kazi na ongezeko la mauzo na masoko”.

Kwa upande wake mwakilishi wa ISO Bw. Nyasha Mupukuta alisema kuwa shirika hilo lilianzishwa kwa dhumuni la kujibu swali la “je ipi ni njia bora zaidi ya kufanya jambo?”


“ISO imetengeneza viwango vinavyozingatia kila sekta hivyo basi kampuni inayopata kuthibitishwa na ISO ina maana kuwa watumiaji wanaweza kuwa na uhakika kwamba bidhaa wanazozitumia ni salama za kuaminika na za ubora wa hali ya juu”. aliongezea Nyasha Mupukuta 

No comments: