Tuesday, March 27, 2018

MECHI YA MBEYA CITY NA YANGA YAPIGWA TAREHE SOMA HAPA KUJUA ..


Tokeo la picha la mbeya city vs yanga
Mechi namba 199 ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Mbeya City na Yanga iliyopangwa kufanyika Mei 1, 2018 kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya itapangiwa tarehe nyingine.

Uamuzi wa kuipangia tarehe nyingine ni kukidhi matakwa ya Kanuni inayotaka nafasi kati ya mechi moja na nyingine isiwe chini ya angalau saa 72.

Kwa mujibu wa ratiba, Yanga itakuwa na mechi dhidi ya Simba itakayofanyika Aprili 29, 2018 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

IMETOLEWA NA BODI YA LIGI KUU TANZANIA

No comments: