Thursday, March 22, 2018

USIPITWE NA NENO WALILOPEWA WANAWAKE WOTE TANZANIA LEO

 Wanawake wametakiwa kupigania haki zao lakinI pia kuwaheshimu waume zao na kulea watoto wao katika maadili mazuri
Ameyasema hayo bi Zuena Saalum Abed mwanzilish wa madrasa ya  swafat mukarama iliyoko Boko jinini Dar es salaam  katika kongamano la wanawake wa kiislam lililofanyika katika Shule ya unio na kuwasii wanawake kusoma na kufuata maadili ya dini kwan kuporomoka kwa maaadili kunachangiwa na wazazI mwenyewe kutowahimiza watoto wao  kwenda kwenye mafunzo ya dini
Wakati huo huo ameomba kwa waislam wenye uwezo kujitolea katika Madrasa iyo kwan wanampango wa kujenga msikiti lakini hawana uwezo pia amewaomba wanaume kuwa na tabia ya kuwaruhusu wake zao kuhudhuria katika makongamano mbali mbali ya kidini kwani husaidia wanawake kukumbuka wajibu wao Katika familia zao
  Nae Ally Mohammad ambae ndie aliefungua kongamano Ilo amesema ni vyema wanawake waungwe mkono katika mambo kama hayo ili kukumbushana wajibu wao katika familia zao na kujua haki zao katika misingi ya kidini.
Njuma maulid ni moja ya mshiriki wa kongamano hilo amesema amefaidika Sana na kongamano hilo kwan limemsaidia kukumbuka wajib wake kama mama katika familia na kama Mke kwani wanawake wengi wa sasa wanatumia muda wao mwing katika kutafuta rizki na kusahau majukumu yao mengine kama mama au Mke hali inayopelekea watoto kutokuwa na maadili mazuri.

No comments: