Thursday, March 22, 2018

MAMA WA MAPACHA WATATU ATELEKEZWA NA FAMILIA BAADA YA MUMEWE KUFARIKI,AOMBA MSAADA WA WATANZANIA

Mila ,desturi na elimu Katika Mtaa wa Basihaya Jijini Dar es salaam zimekuwa changamoto katika Mtaa huo kwani hata katika baadhi ya utatuzi wa matizo mbali mbali ya unyanyaswaji wa wanawake.
              Marinus Albert ndule Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Basihaya ameyasema hayo wakati akiongea na habari 24 jijini Dar es salaam na kusisitiza kuwa ni vyema elimu ya jensia ikatolewa kuanzia ngazi ya Shule ya msingi kwani itasaidia watoto katika ukuaji wao kujua haki zao
Marinus Albert ndule Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Basihaya 
       Pia amesema ni vyema elimu hiyo wakapewa watu wa jinsia zote wanaume na wanawake kwani kumpa mwanamke peke yake  hakutasaidia kuondoa tatizo hilo

      Ameongeza kwa kuwaomba wanawake kuripoti katika vituo vya sheria pindi wafanyiwapo uonevu kisheria na kusisitiza kwa kuomba msaada kwa serikali kumsaidia Bi Veronika Lukasi ambae ni mama wa pacha Watatu 

   Veronika ambae ni mjane na alifiwa na mume we akiwa na ujauzito wa mwezi mmoja na hatimaye alijifungua mapacha Watatu lakin hana msaada kutoka upande wowote na familia yake hawana uwezo kadhalika familia ya marehemu mumewe  hawana uwezo 

 Bi Veronika ameomba msaada kwa serikali kwan hana makazi ya kuishi na watoto wake hao na wakati huo amepata tatizo la ugonjwa wa moyo.

No comments: