Watanzania wametakiwa
kupendana kushirikiana na kushikamana bila kuangalia itikadi ya dini zao ili
kuendelea kuenzi amani na upendo uliopo nchini kwa sasa.
Hayo yamesemwa
mapema leo jijini Dar es salaam na Kiongozi Mkuu wa Dhehebu la Shia nchini
Maulana Hemed Jalala, ikiwa leo maadhimisho ya siku ya Meraji duniani kote.
Sheikh Jalala
alisema kuwa siku ya Meraji ni siku ya kuhamasisha amani na upendo vilivyopotea
katika nchi Palestina, kwani mitume wote walioishi katika ardhi hiyo walikuja
kwa lengo moja la kuleta amani katika nchi hiyo na dunia kwa ujumla.
Aidha Maulana huyo aliendelea kusema kuwa siku ya Meraji ni siku ya mshikamano kwa watu wa dini
zote ikiwemo Waislamu, Wakristo na Wayahudi kwa pamoja kuendelea kutetea na
kulinda amani na mshikamano vilivyopotea ndani ya nchi ya Palestina.
Mkutano ukiendelea. |
Pamoja na
hayo Sheikh huyo alisema kuwa nchi ya Palestina ni nchi ya kihistoria kwa kuwa mitume
wengi waliotumwa na mungu waliishi hapo akiwemo Isaka, Yakubu Mtume Mohamad (S.A.W)
na hata Ibrahimu Baba wa mataifa yote alizikwa katika ardhi hiyo.
“Lakini pia
vitabu vinavyotumiwa na dini zote kubwa ikiwemo Injiri, Torati, Zaburi, na hata
Quran vilishuka katika nchi hiyo na vinaimiza Amani Upendo na Ushirikiano,
hivyo basi kama binadamu tunajukumu kubwa la kuhakikisha vitu hivyo wanavipata
wananchi wanaoishi Palestina”. alisema Sheikh Jalala
Akiongea kwa upande wa Watanzania alisema kuwa Watanzania tukiwa na sifa ya kuwa kisiwa cha Amani tunapaswa kuilinda na kuitetea Amani yetu tusikubali Amani hii ikapotea kirahisi rahisi na tuzidi kuwaombea viongozi wetu watuongoze katika haki na usawa ili kuendelea kuilinda Amani yetu.
"katika kuangalia haya yote yanayotokea nchini ya Palestina kwa sasa sisi kama watanzania tunajifunza kwa namna gani tuilinde na kuitetea amani na yetu na tusikubali kuipoteza kwani ni Tunu tuliyopewa na Mwenyezi Mungu" alisisitiza Sheikh Jalala
No comments:
Post a Comment