Friday, April 13, 2018

Vibe la Tigo Fiesta lapagawisha Sumbawanga

 Wakazi wa manispaa ya Sumbawanga na vitongoji vyake usiku wa kuamkia leo walipata burudani ya aina yake ya msimu wa tamasha kubwa nchini la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote.
Hili ni tamasha la pili kwa mkoa huo baada ya ufunguzi uliofanyika mkoa wa Morogoro.
Msimu huu si kwa burudani tu, bali huwa na fursa mbalimbali kwa wafanyabiasha na waendesha bodaboda.
Kwenye steji ndio kunaacha gumzo kwa wakazi wa miji mbalimbali ambapo tamasha linafanyika.
Akifungua pazia la tamasha hili msanii Nedy Music alianza kuwapasha joto mashabiki akifuatiwa na msanii WhoZu ambaye aliwapagawisha kwa kibao chake kiitwacho "uendi mbiguni".

Msanii mkongwe Farid Kubanda Fid Q nae alichota hisia za mashabiki kwa kushusha nyimbo zake tofauti tofauti ukiwemo Fresh.
Ben Pol ambaye miaka yote huwa mbunifu kwenye jukwaa, alipanda na wenyeji 6 wa mji huo kwa kuonyesha namna ya wakaazi wa Sumbawanga wanaishi katika mazingira tofauti kulingana na anachofanya kwa siku.

Kwa upande wa mdhamini mkuu wa Tigo Fiesta 2018, Mkurugenzi wa Tigo Nyanda za Juu Kusini, Henry Kinabo alisema msimu kampuni ya Tigo imekuja ofa kabambe kwa wateja wao. " Huu ni msimu wa aina yake kama utannunua tiketi kwa Tigo Pesa Master Pass QR utaweza kupata tiketi kwa shilingi elfu tano ambapo ukinunua kawaida unapata kwa elfu saba, kadhalika wateja wa Tigo waingia kwenye shindano la Tigo Fiesta 2018 Chemsha Bongo Trivia, ambapo zawadi za kila siku za shilingi laki moja na za will za milioni 1 utolewa. Pia wateja wa Tigo wataweza kufutahi Huduma ya intaneti kupitia promosheni ya Data Kama Lota kwa kununua kifurushi na kupata mara mbili ya ulichonunua kupitia menu ya *147*00#.

Kesho jumapili Vibe la Tigo Fiesta litahamia mkoani Iringa kwenye uwanja wa Samora na itapandisha wasanii akiwemo Fid Q, Ben Pol,Maua Sama, WhoZu, Marioo, Nandy, Chege,Barnaba, Billinas, Weusi na wengine wengi.

No comments: