Monday, July 18, 2022

Chuo kikuu SUZA kuja na Shahada ya Uzamivu kwenye Sayansi ya Teknolojia ya Habari(IT)

Mkuu wa Kitengo Cha Uhusiano na Masoko wa Chuo Kikuu cha Taifa Cha  Zanzibar( SUZA) Khadija Sadiq Mahumba ( mwenye kitambaa cheupe kichwani)akitoa maelekezo Kwa baadhi ya Wanafunzi waliotembelea Banda la chuo hicho kwenye maonyesho ya 17 ya Tume ya Vyuo Vikuu Nchini ( TCU) katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.
Baadhi ya watu waliotembelea Banda la Chuo kikuu cha Tifa Zanzibar SUZA wakisikiliza maelekezo kutoka kwa Maafisa Udhahili wa chuo hicho wenye Tshirt za rangi ya bluu.

Chuo Kikuu cha Taifa Cha Zanzibar(SUZA) kinaendelea kuunga mkono sekta ya elimu nchini Kwa kuanzisha kozi mpya ambazo ikiwemo ya  Shahada ya Uzamivu kwenye Sayansi ya Teknolojia ya Habari(IT) katika mwaka wa Masomo 2022/ 2023.

Ameyazungumza hayo Mkuu wa Kitengo Cha Uhusiano na Masoko wa SUZA Khadija Sadiq Mahumba wakati akizungumza na Waandishi wa habari kwenye Maonyesho ya 17 ya Elimu ya Juu,Sayansi na Teknolojia yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia kupitia Time ya Vyuo Vikuu Nchini( TCU) Mnazi mmoja jijini Dar es salaam.  

Aidha amesema kwamba chuo hicho kinatarajia kudahili wanafunzi wapatao 2000 Kwa programu mbalimbali zikiwemo za Elimu,Afya,Kilimo kwa ngazi mbalimbali ikiwemo  Cheti,Astashahada( Diploma) Shahada(Degree),Shahada ya Uzamili na Uzamivu.

Amesema kuwa kwa mwaka huu wa masomo chuo hicho pia kinatarajia kutoa programu ya Shahada ya Uzamivu( Phd) ya Lugha ya kiswahili ,na kwamba amewaomba wanafunzi wanaotaka kujiunga na SUZA wachangamkie fursa hizo.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Uhusiano na Masoko SUZA amesema kwamba Chuo hicho kinatoa programu za Kozi za Utalii ambapo wanafunzi watakaosoma kozi hizo watapata fursa ya kusoma lugha mbalimbali za kigeni ikiwemo lugha ya Kireno,Kichina ,Kifaransa,Kijerumani,na kwamba chuo hicho pia kinatarajia kuanza kufundisha Programu ya lugha ya Kikorea.

Hata hivyo amebainisha kuwa wakati wa udahili wa dirisha la pili wanatarajia kudahili wanafunzi kwa program mpya za Shahada ya Uzamili ya Benki na Fedha( MSc Benking & Finance) pamoja na Shahada ya Uzamili ya  Utawala wa Fedha na Biashara ( MBA-Finance).

" Ningependa kuwaomba wazazi wawalete wanafunzi  kwenye banda letu hapa Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam wajionee kozi tunazofundisha ili wafanye maamuzi sahihi yakujiunga na chuo chetu chenye fursa ya kupata ajira nje na ndani ya nchi" amesema Khadija.

No comments: