Monday, July 18, 2022

Chuo Kikuu cha Katoliki Ruaha (RUCU) kimekuja na mambo haya mazuri katika maonyesho ya 17 ya Vyuo vikuu.

Mkurugenzi wa Kozi za Shahada na zisizokuwa za Shahada wa Chuo Kikuu cha Katoliki Ruaha( RUCU) Dkt Wille Migodela (wakatikati) akifuatilia maelekezo yanaoyotolewa na mmoja wa maafisa wa udahili wa Chuo hicho Kwa mwanafunzi aliyetembelea banda hilo kwenye maonyesho ya 17 ya Tume ya Vyuo Vikuu Nchini( TCU), yanayofanyika Viwanja vya  Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Kozi za Shahada na zisizokua za Shahada wa Chuo Kikuu cha Katoliki Ruaha( RUCU) Dkt Wille Migodela (wa kwanza kutoka kushoto) akitoa maelekezo kwa baadhi ya Wanafunzi waliotembelea banda la Chuo hicho kwenye maonesho ya 17 ya Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU) yanafofanyika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.

Chuo Kikuu cha Katoliki Ruaha (RUCU) katika kuhakikisha kinakabiliana na changamoto zinazoikabili Jamii kimejikita kutoa Elimu kwa wanafunzi Kwa kufanya ubunifu wa tafiti mbalimbali Kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za kimazingira Kama vile Mbu wanaoambukiza Ugonjwa wa Malaria.

Magonjwa Mengine ni magonjwa ya ngozi( Fangasi) na Kikohozi,ambapo wanafunzi wanafanya tafiti kupitia mimea ya asili nakutengeneza dawa ambazo zinasaidia kukabiliana na magonjwa hayo.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Kozi za Shahada na zisizo za Shahada wa Chuo hicho Dakt Wille Migodela wakati akizungumza na Waandishi wa habari kwenye maonyesho ya 17 ya Elimu y juu Sayansi na Teknolojia yaliyoandaliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Nchini ( TCU).

Aidha amesema kwamba chuo hicho kinatoa program za Kozi mbalimbali lakini Elimu ya utafiti wa Ubunifu imekua ikipewa kipaumbele ili kumsaidia mwanafunzi anaehitimu kuondokana na zana ya kutemea kuajiliwa na badala yake aweze kujiajiliwenyewe.

Hata hivyo amendelea kusema kwamba Wanafunzi hao wamefanikiwa kubuni kifaa kinachopima uzito wa mizigo inayobebwa na magari ambapo kifaa hicho kinafungwa kwenye gari na gari hiyo haitapita kwenye mzani Kwa ajili ya kupimwa, badala yake kifaa hicho kitaonyesha ukomo wa  uzito kamili unaohotajika kubebwa na gari hilo.

"Magari yanatumia muda mrefu kukaa kwenye foleni ya mzani kupima uzito wa mzigo,sisi kama RUCU tumekuja na suluhisho la kubuni kifaa Cha kisayansi kitakachoonyesha ukomo wa uzito wa mzigo unaotakiwa kupakiwa" amesema Dkt Migodela

Nakuongeza kuwa "kuhusu Faculty of Arts and Social  science ,tumetengeneza kifaa kinaitwa "Analogy wheel" kazi yake ni kupima umbali kwenye tambarare(horizontal distance) wakati wa kufanya Survey(upembuzi).
Kifaa kinafanya kazi mbadala wa Chain(mnyororo) ambao kwa mda mrefu umekuwa ukishindwa kutupa vipimo halisi kwasababu ya masikio(oval shape) yanayo uunganisha na pia chain inatumia mda mrefu kupima urefu ardhini.

Amesema kwamba Kwa mwaka huu wa masomo 2022/ 2023 wanatarajia kudahili  wanafunzi wapatao 1400 ambapo wanafunzi wa Cheti na Diploma ni 700 na wengine 700 ni Shahada(Digree),ambapo amesisitiza kwamba mazingira ya kujisomea Kwa wanafunzi ni mazuri.

No comments: