Tuesday, July 12, 2022

TIC YATOA TATHIMINI YA MAONESHO YA SABASABA 2022, YATANGAZA MAFANIKIO YA MFUMO MPYA WA ‘ELECTONICS INVESTIMENT WINDOW’

Na: Hughes Dugilo, DAR ES SALAAM.
Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) John Mnali ametoa rai kwa wawekezeji wote wa ndani na nje ya nchi kutumia fursa ya Mfumo mpya wa Kielectonic kupata huduma mbalimbali ikiwemo kuomba Vibali na Leseni za Biashara ikiwemo ya uwekezaji na kwamba mfumo huo umelenga kuwawezesha wawekejazi kupata huduma zote kwa wakati mmoja.
 
Mnali ameyasema hayo Julai 12,2022 alipokuwa akitoa tathimini ya maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba yanayotarajiwa kufungwa rasmi Julai 13,2022 katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam ambao amesema kuwa Mfumo huo ujulikanao kama ‘TANZANIA ELECTONICS INVESTIMENT WINDOW’ umewezesha kuunganisha taasisi 6 kwa awamu ya kwanza na kwamba baadae wanatarajia kuongeza taasisi nyingine 11 zitakazofanya kazi kwa pamoja.
 
Ameeleza kuwa katika mfumo huo mwekezaji anaweza kuleta maombi yake kwa njia ya mtandao au kutoa taarifa ya kuhama kutoka eneo moja kwenda eneo jingine, au kurekebisha cheti chake na kwamba kwa kupitia mfumo kunamfanya  mwekezaji kuondokana na usumbufu wa kutembea katika kila ofisi kufuata huduma.
 
“Huduma ziko kwa wawekezaji wote wa ndani na wa nje hivyo itakuwa vizuri kutumia fursa hii kuweza kuandikisha miradi yao, na kufanya maombi yao katika maeneo mambalimbali yanayohitaji huduma katika taasisi husika” 
 
“Kituo cha Uwekezaji tunafahamu kuna miradi mingi sana ambayo inafanyika na wawekezaji wa ndani ambayo haina cheti cha uwekezaji ukizingatia hali ya miradi yao jinsi ilivyo na ukubwa wake inastahili kupata cheti cha uwekezaji.
 
“Elimu hii tuliyoitoa hapa kwa siku zote hizi za maonesho ni vizuri sasa wananchi wanaotaka kuleta maombi mbalimbali watumie mfumo huu kuleta maombi yao, hii itawarahisishia sana kupata huduma kwa haraka” amesema 
Ameongeza kuwa ushiriki wao katika maonesho ya mwaka huu umekuwa wa mafanikio makubwa kutokana na kuwa na maeneo matatu waliyoshiriki ikiwemo Kliniki ya Biashara, uwepo wa eneo maalum la kuonesha utendaji kazi wa mfumo mpya wa ‘ELECTONICS INVESTIMENT WINDOW’, pamoja na ushiriki wao wa jumla ndani ya Banda la Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara lililojumuisha taasisi zote zinazofanyakazi chini ya Wizara hiyo.
Amewataka wananchi wote kutembelea katika ofisi zao za Kanda zilizowekwa kwaajili  ya kutatua changamoto mbalimbali za wawekekezaji waliopo nje ya Jiji la Dar es Salaam, ambapo amezitaja Ofisi hizo kuwa ni pamoja na Kanda ya  Kaskazini,  Nyanda za juu Kusini, Kanda ya Kati na Kanda ya Ziwa.

No comments: