Sunday, December 3, 2017

Meya wa jiji la Dar Mwita ahudhuria mkutano wa kujadili utawala bora Nchini Marekani

MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita leo ameondoka jijini hapa kuelekea Chicago Nchini Marekani kuhudhuria mkutano wa Mameya kutoka sehemu mbalimbali duniani utakaofanyika Desemba 4 hadi 7 mwaka huu.

Mkutano huo unatarajiwa kuhusisha Mameya 182 kutoka sehemu mbalimbali Dunia ambapo pamoja na mambo mengine watajadili suala la utawala bora pamoja na utumishi wa viongozi kwa wananchi.

Aidha katika mkutano huo pia wataangalia na kujadili changamoto za majiji makubwa hususani katika sekta ya Afya, miundombinu, Maji safi na salama, Elimu pamoja na mabadiliko ya tabia ya Nchi.

Desemba  5 Mameya wote waliohudhuria mkutano huo kwa pamoja watashindanisha majiji yaliyofanya vizuri katika sekta ya miundombinu ambapo jiji la Dar es Salaam limeingia kwenye ushindani huo kupitia  mradi wa mabasi yaendayo haraka.

Aidha katika ushindani huo, Meya Mwita amesema kuwa ana amini kwamba jiji la Dar es Salaam litaibuka mshindi wa tuzo hiyo kwa kuwa mradi huo umekuwa ukifanya vizuri katika sekta ya  usafirishaji na kwamba watanzania wajiandae kwa ajili ya kupokea tuzo hiyo.

Majiji mengine ambayo yanameingia kwenye ushindani huo mbali na jiji la Dar es Salaam ni Mji wa Cape Town, Cairo pamoja na majiji mengine Dunia. Meya Mwita atarajea Nchini Desemba 8 mwaka huu.

Imetolewa leo Desemba 3

Na Christina Mwagala, Afisa Habari Ofisi ya Mstahiki Meya wa jiji.


                       

Saturday, December 2, 2017

MAJIMBO YALIYOINGIA KATIKA UCHAGUZI JANUARY 13 JIMBO LA NYALANDU NDANI

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza ratiba ya uchaguzi mdogo katika majimbo ya Singida Kaskazini, Longido na Songea Mjini na kata sita za Tanzania Bara ambao utafanyika Januari 13 mwakani.
Picha inayohusiana
Akitoa taarifa kwa umma jijini Dar es Salaam leo Jumamosi, Makamu Mwenyekiti wa NEC, Jaji mkuu mstaafu wa Zanzibar, Hamid Mahmoud Hamid amesema tume imetangaza uchaguzi huo baada ya kupokea barua kutoka kwa Spika ya kwamba nafasi ziko wazi.

Jimbo la Singida Kaskazini liko kutokana na kujivua  uanachama wa CCM aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Lazaro Nyalandu, Songea Mjini baada ya kifo cha Leonidas Gama na Longido baada ya Mahakama kufuta matokeo ya uchaguzi yaliyokuwa yamempa ushindi Onesmo Ole Nangole.

Akizungumzia uchaguzi wa kata sita amesema waziri mwenye na serikali za mitaa kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292, aliitaarifu Tume kuwepo nafasi wazi za madiwani katika kata hizo Tanzania Bara

Alizitaja kata zinazohusika katika uchaguzi huo kuwa ni Kimandolu(Arusha), Kihesa (Iringa), Bukumbi (Uyui), Kurui (Kisarawe), Keza (Ngara) na Kwagunda (Korogwe).

Amesema utoaji fomu za uteuzi katika majimbo hayo na kata hizo sita utakuwa ni kati ya Desemba 12 hadi 18, 2017 wakati katika jimbo la Songea Mjini utoaji fumo utakuwa kati ya Desemba 14 hadi 20 mwaka huu.

Alifafanua kuwa kwa upande wa kampeni za uchaguzi huo katika majimbo ya Singida Kaskazini na Longido na kata zote sita zitaanza Desemba 19 na kumalizika Januari 12. 

Katika jimbo la Songea Mjini, amesema kuwa kampeni za zitaanza tarehe 21 Desemba, 2017 na kumalizika tarehe 12 Januari, 2018 wakati siku ya uchaguzi katika majimbo yote matatu na kata zote sita itakuwa tarehe 13 Januari, 2017.

Jaji Hamid alivikumbusha vyama vya siasa na wadau wote wa uchaguzi wazingatie sheria, kanuni, taratibu, miongozo na maelekezo yote wakati wa kipindi cha uchaguzi mdogo wa majimbo hayo na kata sita.

MBUNGE MWINGINE WA CUF ASALITI CHAMA NA KWENDA CCM

Mbunge wa Kinondoni jijini Dar, Maulid Mtulia (CUF) leo ametangaza kujiuzulu ubunge na kujivua uanachama wa Chama cha Wananchi CUF na kuhamia CCM.Tokeo la picha la maulid mtulia
Katika barua yake ya kujiuzulu, Mtulia amesema kuwa ameamua kufanya uamuzi huo leo Disemba 2, kwa utashi wake bila shinikizo la mtu yeyote.

Mtulia ameelezea sababu za kujiuzulu nafasi yake hiyo ya ubunge na kuhama chama kuwa imetokana na uzoefu alioupata kwa miaka miwili ya ubunge, na kusema “nimebaini kuwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho ni chama tawala inafanya kazi kubwa ya kutekeleza Ilani na imefanya vizuri katika mambo mengi ambayo sisi upinzani tuliahidi kuyatekeleza” alisema.

Aidha Mbunge huyo amesema kuwa nia yake ni kuwatumikia wananchi, na haoni sababu ya kuendelea kuwa upinzani na badala yake anaona ni vema aungane na juhudi za Serikali, kwa kumuunga mkono Rais Dk. John Magufuli katika kuwaletea wananchi maendeleo na kukabiliana na kero mbalimbali.

Mtulia amesema anawashukuru wananchi wa Jimbo la Kinondoni, kwa kumpa dhamana ya ubunge, katika uchaguzi mkuu uliopita na amewaahidi kuwa yupo tayari kuendelea kushirikiana nao katika maendeleo, akiwa katika uwanja mwingine wa siasa ambao ni Chama Cha Mapinduzi.

DK. KIGWANGALLA AAGIZA NDANI YA SIKU 30 KUJITOKEZA WAMILIKI WA MAGOGO YALIKAMATWA BANDARINI DAR

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla (MB) ametoa muda wa siku 30 kwa wahusika ambao ni wamiliki wa magogo yaliyokamatwa katika bandari ya Dar e s  Salaam (TPA) ambayo yalikuwa yasafirishwe nje ya Nchi, kujitokeza haraka kueleza wameyato wapi na walikuwa na lengo gani baada ya kuyatelekeza bandarini  hapo kwa muda wa miaka 10 sasa huku mengine yakitelekezwa pasipo kuwa na vibali maalum.
Dk.Kigwangalla ametoa kauli hiyo baada ya kufanya ziara ya ghafla bandarini hapo kukagua mali na bidhaa zinazoshughulikiwa na Wizara yake hiyo ambapo katika zkukagua kwake huko alibaini uwepo wa makontena hayo 55 ambayo yapo  kwa miaka 10 sasa yakihifadhiwa huku wahusika wakishindwa kujitokeza.
“Naagiza mamlaka zilizo chini ya wizara yangu kuhakikisha wanahakiki magogo yote yalipo hapa bandarini. Mwenye huu mzigo lazima ajulikane hasa haya magogo 938, Ndani ya siku 30 mwenye haya magogo atangaziwe na ajitokeze vinginevyo itabaki kuwa mali ya Serikali” alisema Dk. Kigwangalla.
Hata hivyo aliagiza pia kontena 55 zilizokutwa bandarini hapo zenye magogo pia nazo wahusika wajitokeze na nyaraka zao kamili ili waeleze kama kweli wameyatoa  Zambia magogo hayo ama sehemu gani hivyo wajitokeze na wasipofanya hivyo ndani ya siku hizo 30, magogo hayo yatataifishwa na kuwa mali ya Serikali.
Katika ziara hiyo, Waziri Dk.Kigwangalla aliweza kutembelea bandari ya Dar es Salaam pamoja na maeneo yanayohifadhiwa magogo hayo zikiwemo bandatri ya nchi kavu ya NASACO, Malawi (Malawi Cargo) na baadae eneo hilo la bandari ya Dar es Salaam.
Akiwa katika eneo la Malawi Cargo, Waziri Dk. Kigwangalla aliweza kushuhudia makontena mbalimbali yakiwemo yale ya  mbao aina ya mitiki ambayo inatarajiwa kusafirishwa nje ya nchi huku akibaini uwepo mkubwa wa udanganyifu kwa wasimamizi wa upakuaji na usafirishaji katika eneo hilo la bandari ambao awali walitaja idadi ndogo ya makontena ya mbao mbele ya Waziri hali iliyopelekea kuanza kuyakagua makontena yote ndani ya eneo hilo.
KAWAIDA:
DK. KIGWANGALLA AAGIZA NDANI YA SIKU 30 KUJITOKEZA WAMILIKI WA MAGOGO YALIKAMATWA BANDARINI DAR
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla (MB) ametoa mud wa siku 30 kwa wahusika ambao ni wamiliki wa magogo yaliyokamatwa katika bandari ya Dar e s  Salaam (TPA) ambayo yalikuwa yasafirishwe nje ya Nchi, kujitokeza haraka kueleza wameyato wapi na walikuwa na lengo gani baada ya kuyatelekeza bandarini  hapo kwa muda wa miaka 10 sasa huku mengine yakitelekezwa pasipo kuwa na vibali maalum.
Dk.Kigwangalla ametoa kauli hiyo baada ya kufanya ziara ya ghafla bandarini hapo kukagua mali na bidhaa zinazoshughulikiwa na Wizara yake hiyo ambapo katika zkukagua kwake huko alibaini uwepo wa makontena hayo 55 ambayo yapo  kwa miaka 10 sasa yakihifadhiwa huku wahusika wakishindwa kujitokeza.
“Naagiza mamlaka zilizo chini ya wizara yangu kuhakikisha wanahakiki magogo yote yalipo hapa bandarini. Mwenye huu mzigo lazima ajulikane hasa haya magogo 938, Ndani ya siku 30 mwenye haya magogo atangaziwe na ajitokeze vinginevyo itabaki kuwa mali ya Serikali” alisema Dk. Kigwangalla.
Hata hivyo aliagiza pia kontena 55 zilizokutwa bandarini hapo zenye magogo pia nazo wahusika wajitokeze na nyaraka zao kamili ili waeleze kama kweli wameyatoa  Zambia magogo hayo ama sehemu gani hivyo wajitokeze na wasipofanya hivyo ndani ya siku hizo 30, magogo hayo yatataifishwa na kuwa mali ya Serikali.
Katika ziara hiyo, Waziri Dk.Kigwangalla aliweza kutembelea bandari ya Dar es Salaam pamoja na maeneo yanayohifadhiwa magogo hayo zikiwemo bandatri ya nchi kavu ya NASACO, Malawi (Malawi Cargo) na baadae eneo hilo la bandari ya Dar es Salaam.
Akiwa katika eneo la Malawi Cargo, Waziri Dk. Kigwangalla aliweza kushuhudia makontena mbalimbali yakiwemo yale ya  mbao aina ya mitiki ambayo inatarajiwa kusafirishwa nje ya nchi huku akibaini uwepo mkubwa wa udanganyifu kwa wasimamizi wa upakuaji na usafirishaji katika eneo hilo la bandari ambao awali walitaja idadi ndogo ya makontena ya mbao mbele ya Waziri hali iliyopelekea kuanza kuyakagua makontena yote ndani ya eneo hilo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangallaakitoa maagizo kwa uongozi wa bandari ya TPA.
Baadhi ya magogo hayo yaliyokutwa katika makontena bandarini hapo
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla wakiwa katika eneo la bandari ya nchi kavu ya Malawi Cargo. wakati wa kukagua magogo hayo
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua baadhi ya mbao zilizokutwa bandarini hapo katika eneo la Malawi Cargo
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua baadhi ya mbao zilizokutwa bandarini hapo katika eneo la Malawi Cargo
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akionyeshwa nyaraka ya idadi ya makontena  katika eneo la Malawi Cargo
Zoezi la ukaguaji likiendelea
Baadhi ya magogo yaliyokutwa bandarini hapo

Meya Mwita ashangaa watu wa Kisiwa Cha Mayotte wakizungumza Kiswahili.

MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa watu 10 kutoka Kisiwa cha Mayotte kilichopo Nchini Ufaransa.

Ujumbe huo ulikuwa umeambatana na wabunge watatu kutoka Nchini humo, Rais wa Shirikisho la wafanyabiashara wa Mayotte pamoja na wajumbe wengine ambao ni wawakilishi kutoka kampuni mbalimbali kisiwani humo.

Katika mazungumzo hayo, Mstahiki Meya Mwita na wageni wake wamejadili mambo mbalimbali ya maendeleo jijini hapa hususani masuala ya kibiashara ambapo amewakaribisha na kuahidi ushirikiano kwao.

Aidha Meya Mwita pia ameshangaa kuona ugeni huo kutoka Kisiwa cha Mayotte wakizungumza Kiswahili jambo ambalo alidai kuwa ni la kihistoria kutokana na historia ya Nchi hiyo.

Kutokana mshangao huo, ambao uliambatana na furaha ndani yake, aliwakabidhi zawadi ya Kamusi ya Kiswahili kwa lengo la kuendelea kujifunza zaidi Lugha ya Kiswahili pindi watakaporejea nchini kwao.

“ Nimefarijika na kushangaa baada ya kusikia asilimia 40 ya wananchi wakisiwa cha Mayote wanazungumza lugha ya Kiswahili, hii ni ajabu, lakini inaonyesha ninamna gani ambavyo watu wanaipenda Lugha yetu” amesema Meya Mwita.

Awali jumbe huo ulikutana na kufanya mazungumzo na Shirikisho la wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo Tanzania.

Imetolewa leo Desemba 1 na Christina Mwagala, Afisa habari Ofisi ya Meya wa jiji.

Rais wa Shirikisho la wafanyabishara na Viwanda  wa Mayotte Nchini Ufaransa Hamidani Magoma akimuelekeza jambo kwenye kwenye dokomenti Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita walipomtembelea ofisini kwake na kujadili mambo mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya biashara jijini hapa.


Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita wa kwanza kushoto, akimsikiliza Rais wa Shirikisho la wafanyabishara na Viwanda Hamidani Magoma mwenyemiwani  walipokutana katika ofisi za Mastahiki Meya jiji.


Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Saalam Isaya Mwita akimkabidhi Rais wa Shirikisho la wafanyabishara na Viwanda  wa Mayotte Hamidani Magoma Kamusi ya Kiswahili baada ya kuzungumza Kiswahili.


Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita watatu kulia mstari wa mbele akiwa kwenye picha ya pamoja na ujumbe kutoka Kisiwa Cha Mayotte kilichopo Nchini Ufaransa walipomtembelea ofisini kwake.

Friday, December 1, 2017

ALICHOKISEMA NYALANDU KUHUSU BIASHARA YA UTUMWA INAYOENDELEA NCHINI LIBYA

Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na Mbunge wa wa Singida Kaskazini aliyejiuzulu, Lazaro Nyalandu ameutaka Umoja wa Mataifa kuchukua hatua zaidi juu ya kinachoendelea nchini Libya.
Tokeo la picha la nyarandu
Amesema kuwa ni lazima hatua zichukuliwe kwa kile kinachoendelea nchini Libya ili kuweza kukomesha kile ambacho kinaendelea kwa sasa dhidi ya binadamu.

“Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika lazima uchukue hatua dhidi ya Libya sasa. tunachoshuhudia ni matusi kwa wanadamu,”amesema Nyalandu

Aidha, siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa zikiripotiwa kutoka Libya kuwa kumekuwa na biashara ya utumwa ikifanyika ikihusisha Libya kuuza Waafrika nchi za Ulaya.

Ubalozi wa Libya nchini Tanzani umesema kuwa Waafrika wanaodaiwa kuuzwa kutoka nchi hiyo, yawezekana walikuwa wanakabidhiwa kwa watoroshaji ili wawapeleke Ulaya na sio kuwauza kama watumwa.

WEMA SEPETU AWEKA WAZI SABABU ZA KUHAMA CHADEMA NA KURUDI CCM

Miss Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu ametangaza rasmi kujivua uanachama wa Chadema na kurudi kwenye chama chake cha zamani cha CCM.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Wema Sepetu amesema hawezi kuishi kwenye nyumba inayomkosesha amani ya nafsi.

“Siwezi Kuendelea kuishi kwenye Nyumba inayo nikosesha amani… Peace of mind is everything for me… Natangaza Rasmi kuondoka Chadema na Kurudi Nyumbani“ameandika Wema Sepetu kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Mapema mwezi Februari mwaka huu mrembo huyo alitangaza kuihama CCM na kujiunga Chadema akisema “Nimeamua kufanya uamuzi wa kuhama chama cha Mapinduzi na hivi sasa nataka kuhamia Chadema. Sitaki ionekane kwamba labda nimepata hasira kulingana na hizi tuhuma za hapa katikati ambazo zimenikabili. 

Lakini nataka nionekane nimefanya maamuzi kama binadamu yeyote ambaye angeweza kufanya. Nadhani wote mnajua kuwa nilishawahi kuwa kada wa Chama cha Mapinduzi, nilikuwa nalisema kwa kujiproud nikiwa nina uaminifu mkubwa kwamba mimi nitasimama kama kweli kada wa Chama cha Mapinduzi”

MHE MWANJELWA AIPONGEZA NFRA KUANZISHA MRADI WA KUONGEZA UWEZO WA KUHIFADHI MAZAO KUPITIA UJENZI WA VIHENGE NA MAGHALA NCHINI

Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo mara baada ya kutembelea Ghala la Wakala Wa Taifa Wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Kanda ya Makambako, Mkoani Njombe wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja, Leo Novemba 1, 2017. Picha Zote Na Mathias Canal
Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza na Wakulima wa Mji wa Makambako, Mkoani Njombe katika ukumbi wa Wakala Wa Taifa Wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Kanda ya Makambako, Mkoani Njombe wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja, Leo Novemba 1, 2017.
Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua mahindi yaliyohifadhiwa kwenye Ghala la Wakala Wa Taifa Wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Kanda ya Makambako, Mkoani Njombe wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja, Leo Novemba 1, 2017.
Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisikiliza maelezo kutoka kwa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Wa (NFRA) Bi Vumilia L. Zikankuba ya namna ya ununuzi na uhifadhi wa mahindi kwenye Ghala la Wakala Wa Taifa Wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Kanda ya Makambako, Mkoani Njombe wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja, Leo Novemba 1, 2017.

Na Mathias Canal, Njombe

Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa amesifu juhudi za uongozi Wa Wakala Wa Taifa Wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) kwa utendaji kazi kwa ubunifu kwa kuanzisha Mradi Wa kuongeza uwezo Wa kuhifadhi Mazao.

Mradi huo utahusisha ujenzi Wa Vihenge vya kisasa, Mghala ya kisasa pamoja na ukarabati Wa Ofisi ambapo baada ya mradi huo kukamilika wakala utakuwa umeongeza uwezo Wa kuhifadhi Shehena ya mahindi ya uzito Wa zaidi ya Tani 250,000 ambapo Vihenge vya kisasa ni 190,000 MT na Maghala 60,000 MT.

Mradi huo unataraji kutekelezwa na kampuni mbili za kandarasi kutoka serikali ya Poland (Feerum na Unia Arab) kwa usimamizi Wa Wakala Wa Majengo Tanzania (TBA) ambapo unataraji kugharimu zaidi ya Bilioni 150 za Kitanzania.

Tayari maandalizi ya awali yameshakamilika ikiwemo Utiwaji saini mikataba, Uchunguzi Wa udongo, Tathmini ya athari ya Mazingira, Pamoja na kutembelea eneo la mpango kazi.

Akizungumza wakati akikagua Ghala la Kuhifadhia mahindi Kanda ya Makambako Mkoani Njombe, Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa alisema kuwa Wakala Wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) umefanya kazi kubwa ya ubunifu na kujiongeza kwa ajili ya kuwanufaisha wakulima katika Kanda zote saba ikiwemo ya Makambako-Njombe, Kipawa-Dar es salaam, Dodoma, Shinyanga, Arusha, Songea na Sumbawanga.

Alisema kuwa pamoja na Kanda ya Makambako kupangiwa kununua jumla ya Tani 6500 katika msimu Wa mwaka 2017/2018 ambapo baada ya lengo kukamilika ziliongezwa fedha za ununuzi hivyo kununua jumla ya Tani 8,961.530

Akisoma taarifa ya Wakala Wa Taifa Wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Wa (NFRA) Bi Vumilia L. Zikankuba alisema kuwa Kanda ya Makambako ni miongoni kwa Kanda itakayoongezewa uwezo Wa kuhifadhi ambapo tayari kuna kiwanja chenye ukubwa Wa Hekari 2,9965 kilichopo Makambako na Mbozi chenye ukubwa Wa Hekari 53.691.

Alisema Wakala umefanikiwa kutekeleza majukumu yake ikiwa ni pamoja na kununua baadhi ya Mazao ya Chakula cha ziada kutoka kwa wakulima, Kutoa Chakula cha ziada kwa waathirika, Kutekeleza mkakati Wa kukuza uchumi na kupunguza umasikini (MKUKUTA) kwa kutoa bei nzuri kwa wakulima wanaouza Mazao yao kwa NFRA sambamba na utekelezaji Wa malengo ya milenia 2025.

Katika ziara hiyo ya kikazi ya Siku Moja katika Mji Wa Makambako Mkoani Njombe, Naibu Waziri Wa Kilimo pia amekutana na kufanya kikao cha kazi na wafanyakazi Wa Wakala Wa Taifa wa Hifadhi ya chakula Kanda ya Makambako ambapo pamoja na mambo mengine amewasihi kufanya kazi kwa Nidhamu, Weledi, Kujituma, Uvumilivu, Bidii na mshikamano.

Wakati huo huo amefanya mazungumzo na wakulima kutoka Kanda ya Makambako ambapo wakulima hao wamesifu Juhudi za serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe Rais Wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kuwajali ikiwa ni pamoja na kupunguza Tozo na Ushuru.

Wakulima hao kwa nyakati tofauti wameupongeza Uongozi Wa Wakala Wa Taifa Wa Hifadhi ya Chakula Kanda ya Makambako kwa kuwashirikisha na kuwajali wakulima katika kila hatua ya ununuzi Wa mazao.

EfG YAZINDUA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA JIJINI DAR ES SALAAM Inbox x

 Mkurugenzi wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Jane Magigita akihutubia katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia uliofanyika Dar es Salaam jana Soko la Tabata Muslim.
 Mratibu wa Mradi wa Mpe Riziki Si Matusi, Susan Sita akimpatia fulana Mwakilishi wa Mbunge wa Segerea, Bonah Kaluwa aliyefika kwaniaba yake kama mgeni rasmi, Shanisudin Ahmed wakati wa uzinduzi huo.
  Mkurugenzi wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Jane Magigita, akimkaribisha mgeni rasmi katika uzinduzi.
 Mwenyekiti wa Soko la Tabata Muslim, Haji Mohamed akihutubia.
 Mratibu wa Mradi wa Mpe Riziki Si Matusi, Susan Sita, akihutubia.
 Wawezeshaji wa kisheria wa EfG wakiwa na furaha katika uzinduzi huo.
 Burudani ikitolewa.
 Burudani ikiendelea.


 Mkurugenzi wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Jane Magigita akihutubia
 mgeni rasmi, Shanisudin Ahmed, akihutubia wakati wa uzinduzi huo.
 uzinduzi ukiendelea.
 Wadau mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi huo
 Mkurugenzi wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Jane Magigita akiteta jambo na mgeni rasmi.
Mgeni rasmi akijumuika na wadau mbalimbali na wawezeshaji sheria wa shirika hilo.

Na Dotto Mwaibale

SHIRIKA la Equality for Growth (EfG) lenye makao makuu yake jijini Dar es Salaam, jana limezindua siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kama taifa na kuungana na mataifa mengine duniani katika maadhimisho hayo.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika Soko la Tabata Muslim Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa shirika hilo, Jane Magigita amesema kwa sasa EfG inaendesha mradi unaoitwa "MPE RIZIKI SI MATUSI" ambao umeongeza wigo wa mapambano ya ukatili wa kijinsia  katika Wilaya ya Ilala na Temeke katika masoko sita.

Ameyataja masoko hayo kuwa ni Mchikichini, Kisutu,Tabata Muslim, Feri, Gezaulole na Temeke Stereo.

Magigita aliongeza kuwa, lengo la mradi huo ni kuona wanawake wafanyabiashara wa Manispaa ya Ilala na Temeke wanafanyabiashara katika mazingira huru dhidi ya ukatili wa kingono, kimwili, matusi na kisiasa, vilevile kuona wanawake wakipewa heshima kama binadamu wengine ili waweze kujipatia kipato chao bila vikwazo.

"Mbali na kuwepo mashirika mbalimbali yanayojihusisha na masuala ya ukatili wa kijinsia, EfG pekee ndiyo ambayo inajihusisha na kuwasaidia wafanyabiashara katika masoko na kuwapa elimu ya haki za binadamu, sheria na ukatili wa kijinsia," alisema mkurugenzi huyo na kuongeza;

"Hii inaonyesha ni kwa jinsi gani tulivyoweza kutambua kuwa sekta isiyo rasmi inasahaulika ukilinganisha na sekta zingine."

Aidha, Magigita alitumia fursa hiyo kulishukuru Shirika la UN Trust Fund kwa kuwawezesha ili kufikia azma mahususi.

Mkurugenzi huyo wa EfG amesema madhumuni ya kuwepo kwetu hapa leo ni kutokana na azma yetu sote kama taifa na kuungana na mataifa mengine duniani katika kuadhimisha siku 16 za kupinga vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia na pia kuweka msisitizo kwenye utawala wa sheria na upatikanaji wa haki.

"Kama wote tunavyofahamu, chanzo cha maadhimisho haya ni mauaji ya kikatili ya wasichana wa Mirabelle huko nchini Dominika yaliyofanyika mnamo miaka  ya 1960. 
Kutokana na hali hiyo, mwaka 1991, Umoja wa Mataifa ulitenga siku 16 kuanzia Novemba 25 kila mwaka kama siku ya kimataifa ya kuopinga unyanyasaji dhidi ya wanawake. Vilevile, siku ya kuhitimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ambayo ni Desemba 10," alisema.

Ameongeza kuwa, utafiti unaonyesha wanawake wa Dar es Salaam walio katika sekta isiyo rasmi ndiyo kundi ambalo linakumbwa kwa kiasi kikubwa na ukatili wa kijinsia wawapo nyumbani hata wanapokuwa maeneo yao ya kazi.

Pia utafiti unaonyesha wanawake hao, wanakosa ulinzi toka kwa serikali na mamlaka husika.

"Wanawake wafanyabiashara sokoni ni kundi mojawapo la wafanyakazi katika sekta isiyo rasmi walioamua kukataa umaskini na kuingia katika harakati za kuinua uchumi wao na familia zao. 

Utafiti uliofanywa na shirika letu la EfG mwaka 2015 ulionyesha kuwa wanawake katika masoko yetu wanafanyakazi kwenye mazingira magumu na wengi wao wakiendesha biashara duni na zenye ufanisi mdogo.

Akisoma risala hiyo kwa mgeni rasmi, Shanisudin Ahmed ambaye ni Katibu wa Ofisi ya Mbunge wa Segerea aliyemwakilisha Mbunge wa Jimbo la Segerea, Mheshimiwa Bona Kilua ambaye hakufika kutokana na tatizo la kiafya, Magigita alisema;

" Katika masoko kumi yaliyotembelewa  wakati wa utafiti huu uliofanywa kwenye Manispaa ya Ilala na Temeke ulionyesha kuwa asilimia 95.97% ya wanawake wanapitia ukatili wa kijinsia wanapokuwa mahala pa kazi yaani sokoni, wanawake hawa hukosa mitaji ya kutosha wakati wa kuanzisha baishara, wengi hawana elimu ya usimamizi wa biashara na wala hawashiriki katika kufanya maamuzi na kugombea nafasi za uongozi katika masoko pia ilionekana kwamba hawana dhamana kwa ajili ya kuchukua mikopo, hivyo kubaki na zana na vitendea kazi duni vya kuendesha biashara zao," alisema na kuongeza;

"Ukatili ambao umekuwa ukijitokeza mara kwa mara katika masoko ni pamoja na kushikwa maongo ya mwili, lugha chafu na matusi, vitisho, jaribio la kubakwa na kejeli, rushwa ya ngono. Pia utafiti ulionyesha madhara wanayoyapata wanawake hawa katika masoko ambayo ni kushindwa kuzalisha ipasavyo, kuharibika kisaikolojia, kutojiamini, kuwa na hofu, uwoga, kutoheshimika pia kudhalilika," alisema.

Magigita alisema kuwa kupitia mradi wa "MPE RIZIKI SI MATUSI" unaofadhiliwa na Un Trust Fund, shirika limefanikisha kuwafikia wafanyabiashara wapatao 10,250 kwa kuwapa elimu ya ukatili wa kijinsia, sheria na haki za binadamu, kutoa msaada wa kisheria kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia wapatao 1800 ambao mashauri yao yametatuliwa, kutoa rufaa zipatazo 75, masoko 10 yameridhia kuanza kutumia mwongozo wa kupinga ukatili wa kijinsia katika masoko, kugawa machapisho yapatayo 5,500 kwa wafanyabiashara na wadau mbalimbali katika kuongeza uelewa wao.

Ameongeza kuwa, wafanyabiashara wameweza kujitambua na wanajua wapi waende kutoa taarifa pindi wanapofanyiwa ukatili, pia kumekuwepo na ongezeko la utoaji wa taarifa za ukatili wa kijinsia kwa viongozi wa masoko na polisi, maofisa 120 wa vyombo vya ulinzi na usalama wameongeza uelewa juu ya masuala ya ukatili wa kijinsia, sheria na haki za wanawake jambo lililofanya ukatili masokoni kupungua kwa asilimia 81 kwa mujibu wa utafiti wa Machi 2017 hasa lugha ya matusi na bughudha kwa wanawake.

Mkurugenzi huyo amesema, kupitia kauli mbiu ya mwaka huu inayosema; "FUNGUKA! UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO HAUMUACHI MTU SALAMA. CHUKUA HATUA" tunakusudia kutoa elimu kwa wafanyabiashara katika masoko yote ili wasikae kimya wanapofanyiwa ukatili wa kijinsia kwani madhara yake ni makubwa sana na yanarudisha nyuma maendeleo ya taifa letu.

"Ombi letu kwa Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya zinazohusika katika kutoa huduma kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia ni kuwepo mikakati ya wazi kuhakikisha wanawake katika sekta hii wanapewa kipaumbele ili kuwaweka huru na bughudha zote za ukatili dhidi yao. 

Pia ni muhimu kwa vyombo vya utoaji haki vihakikishe kuwa wanawake wanaofanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia wanapata haki na wale wanaohusika katika kutenda vitendo hivyo wanakumbana na mkono wa sheria ili iwe fundisho kwa wengine.

"Kwa hili tunaomba jeshi la polisi lishirikiane kwa ukaribu na watoa huduma wetu ambao hutoa huduma ya rufaa kwa wahanga na wapate fursa za kuongeza kipato na kunia uchumi wa taifa," alisema Magigita.

Naye Ahmed aliyemwakilisha Mbunge wa Segerea akizungumza baada ya kusikia risala hiyo alisema amefarijika sana kuona kuwa ili kuinua uchumi na kutokomeza ukatili wa kijinsia si tu kwa wananchi bali kila mtaalam anachukua nafasi yake ili kutoa mchango wake.

"Hili limenipa faraja kubwa mimi binafsi na serikali kwa ujumla hasa hasa katika kuimalishaaa sekta binafsi, mmeweza kuonyesha kwamba kila Mtanzania anafanya bidii kuchangia katika kuleta maendeleo endelevu katika ukuaji wa sekta isiyo rasmi Tanzania ambayo ipo katika sekta binafsi. Nawashukuru sana EfG kwa kuwa mfano mzuri kwa hili," alisema Ahmed.


Katibu huyo wa Mbunge wa Segerea aliongeza kuwa, Dira ya Taifa inaeleza kuwa Tanzania itakuwa na jamii yenye usawa wa kijinsia ifikapo mwaka 2020. Hatuwezi kufikia dira hiyo tutaruhusu aina ya ukatili wa kijinsia kujitokeza tena au aina mpya kabisa kujitokeza na kukua miongoni mwetu. Tunahitaji kuwa na jamii yenye usawa kijinsia nyakati zote.

"Napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza kwa dhati kwa hatua hiyo kubwa ya kupeleka huduma hizo kwa wafanyabiashara kwani mara nyingi baadhi ya wafanyabiashara hawafikiwi katika maeneo yao ya biashara na hivyo kukosa fursa ya kukosa elimu ya kupambana na ukatili wa kijinsia," alisema Ahmed.


MFUMO WA RAIS WA KUKUSANYA MAPATO KIELEKTRONIKI UMEPEISHA MAPATO YA KODI YA MAKAMPUNI YA SIMU KWA 102%


Mfumo wa Kukusanya Mapato Kielekroniki (eRCS) umeonyesha mafanikio makubwa kwa miezi mitatu ya mwanzo ya Julai, Agosti na Septemba 2017, baada ya Makusanyo ya Kodi kwa Upande wa Zanzibar (ZRB) kupitia eRCS kufikia Shilingi Bilioni.7.2, ukilinganisha na Shilingi Bilioni 3.5, ZRB walizokusanya kipindi Kama hicho mwaka 2016 kabla ya mfumo wa eRCS. Makusanyo hayo yakiwa ni Ongezeko la Shilingi Bilioni 3.6 sawasawa na asilimia102%. Ni zaidi ya Mara mbili ya makusanyo ya mwaka Jana kabla ya mfumo wa eRCS, yanayofikia shilingi Bilioni 7.2 ni majumuisho wa Ushuru wa Bidhaa (Excise Duty) na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) Baada ya kukata Marejesho.
Wakati huo huo Taarifa tulizonazo kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ni kwamba makusanyo ya kodi yanayotokana na kampuni za simu, kwa kutumia eRCS TRA wamefanikiwa kuongeza makusanyo kwa asilimia 21% kwa kukusanya Jumla ya shilingi Bilioni 128.9 kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai, Agosti na Septemba 2017, ukilinganisha na makusanyo ya miezi ya Aprili, Mei na Juni 2017 kabla ya kuanza kutumia mfumo wa eRCS. Aprili, Mei na Juni 2017 kabla ya eRCS, makampuni ya simu saba yalilipa jumla ya kodi ya Shilingi Bilioni 101.7. Julai, Augusti na Septemba 2017, baada ya kuanza kutumika eRCS, Makampuni ya simu yale yale yameweza kulipa Shilingi Bilioni 128.9. Kukiwa na ongezeko la Shilingi Bilioni 27.2 sawa na 21% ambazo ni majumuisho yaliyotokana na kodi ya Ongezeko la thamani (VAT) na Ushuru wa Bidhaa (Excise Duty).
Ukijumuisha makusanyo yanayotokana na Kodi kutoka kampuni za simu saba kuanzia mwezi Aprili 2017 mapaka mwezi Septemba 2017 TRA imekusanya Jumla ya Shilingi Bilioni 230.7. kwa kipindi cha miezi sita tu, ambazo ni wastani wa shilingi Bilioni 38.5 kwa mwezi. Taarifa tulizopata kutoka chanzo chetu ambao hawakutaka majina yao yatajwe wametueleza kwamba Serikali inafuatilia kwa kina udanganyifu unaofanywa na kampuni za simu katika Taarifa zao walizozipeleka TRA za input kwa ajili ya “return” ambazo zinakosa uhalisia kwani zinajumuisha taarifa za miezi iliyopita kwa lengo la kuongeza kiwango cha input tax.
Mfumo eRCS ulizinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar Dkt. Mohamad Shein walipozindua Dirisha la kukusanya kodi Kielekroniki Elecrtronic Revenue Collection System (eRCS) tarehe 1 Juni 2017, ukiwa na lengo la kusaidia Mamlaka zote mbili za Mapato yaani Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRB) kuongeza mapato yanafanyika kupitia njia za kielektroniki. Mpaka Mwezi Novemba 2017, ni kampuni saba za simu ndizo zilizounganishwa katika mfumo wa eRCS, Kampuni hizo ni Vodacom, TTCL, Airtel, tiGO, Halotel, Zantel na Smart. Taarifa hii imeandikwa kutokana na taarifa zinazopatikana IDC, TRA na ZRB Novemba 2017.

HEINEKEN® LAUNCHES AMSTEL BEER IN THE TANZANIAN MARKET

General Manager for Heineken East Africa, Mr. Uche Unigwe (right) delivers keynote speech during the official launch of Amstel lager in Tanzania. Looking on is Country Manager for Heineken Tanzania Michael Mbungu.


General Manager for Heineken East Africa, Mr. Uche Unigwe (second from left) with various stakeholders  during the official launch of Amstel lager in Tanzania. 
HEINEKEN Tanzania today officially announced the launch of premium beer brand AMSTEL into the Tanzanian market. Speaking at the launch event in Dar Es Salaam, HEINEKEN East Africa General Manager Uche Unigwe said the introduction of AMSTEL was advised by the growing demand by Tanzanians for a different brand of quality beer in the market.
“The decision to introduce AMSTEL into the Tanzanian market is informed by our research that shows our target consumer enjoys a classier lifestyle in their everyday pursuit of attainable luxuries”. “This provided a great opportunity for us to expand our portfolio of products thus we brought in AMSTEL to meet this demand”, he said
Uche noted “Premium domestic beer drinkers now have the option of socializing without sacrifice with a beer that instils the confidence of a premium brand choice without losing taste or image.”
The distinctive, golden AMSTEL beer with its mildly bitter taste and excellent quality has become well known around the world, beyond the borders of its native Netherlands. Today AMSTEL is available in over 100 countries. We proudly welcome this new gem to the Tanzanian market.
This entry by AMSTEL will add momentum in transforming HEINEKEN East Africa’s existing business across the country by extending its footprint, increasing scale and further strengthening its brand portfolio” said Michael Mbungu, Country Manager HEINEKEN Tanzania.  He added, “AMSTEL is a winning proposition for retailers and on-premise operators as it offers an imported alternative to their domestic premium beer selection.
HEINEKEN TANZANIA, through the AMSTEL Brand will also participate in a series of in-country partnerships and events to further cement AMSTEL’s winning proposition. Additionally, we are the official sponsors of the Europa League and we plan on bringing the momentum of the beautiful game to the region, as you are aware the Europa League is growing”, he added.
With a brand heritage that spans way over a century, AMSTEL aims to encourage consumers to enjoy their drink and at the same time advocates responsible drinking. Amstel is available at retail outlets countrywide where Tanzanians will get to experience it in a 330ml bottle and a 500ml can.