Wednesday, June 19, 2013

WADAU WA SECTA YA NISHATI WAIKUMBUSHA SERIKALI



          Serikali imeshauriwa kuendelea kuzalisha  umeme kwa njia ambazo ni salama kwa mazingira ikiwa ni pamoja na kuweka kipaumbele katika matumizi ya umeme wa maji na gesi asilia  ambao imetajwa kuwa ndio njia rafiki kwa mazingira
          Wito huo umetolewa katika semina uliowakutanisha wadau mbalimbali wa nishati nchini wenye lengo la kuzindua mpango mkakati wa kuzalisha umeme kwa njia ambazo ni salama kwa nchi kama maji na gesi asilia semina  iliyofanyika jijini dar se salaam.
          Akizungumza katika semina hiyo iliyohudhuriwa na wataalam mbalimbali kutoka wizara ya nishati na madin.wizara ya kilimo,pamoja na wizara sayansi na technologia mwandaaji wa semina hiyo bw LEORNAD KASSANA amesema kuwa ili kutunza mazingira lazima serikali iendeleze jiihata zake za kufua umeme wa maji ambayo ndio njia rafiki kwa mazingira
         Bw KASSANA kuwa serikali ina rasilimali nyingi ambazo kama zitatumika ipasavyo kuzalisha umeme zinawaza kusaidia katika kuokoa mazingira
           Aidha ameongeza kuwa serikali lazima iwashirikishe wadau katika maswala ya nishati salama kwani umeme ndio uti wa mgongo wa uchumi wa tanzania.

No comments: