Thursday, January 23, 2014

CCM YAMTAKA MEYA WA BUKOBA AMAN AONDOKE OFISINI MARA MOJA



 Na Karoli Vinsent.    
 CHAMA chaMapinduzi CCM kimemtaka Meya wa manispaa ya Bukoba  Anatory Amani,kuondoka Ofisini maramoja lasivyo chama hicho kitamchukulia hatua ya kumfukuza uwanachama.
       
    Akitoa ufafanua uamuzi huo  Katibu Mwenezi wa chama cha Mapinduzi CCM, Nape Nnauye,wakati anaongea na mwandishi wa Mtandao huu alisema haoni sababu ya Meya kukaa ofisini hakati teyali ameshaachia ngazi.

    “Mimi mwenyewe nimepigania suala hili sana hadi watu wengine wakaanza kunichukia kuhusu uwajibikaji wangu kuhusu ufisadi wa meya Amani,lakini leo ripoti ya mkaguzi wa Serikali imeonyesha ufisadi mkubwa sana,leo  nashangaa bado yupo ofisini. Jambo la ajabu sana, wakati tayari alishajiuzulu na Barua yake mimi nimeiyona sasa anatafuta nini ofisini”alisema Nnauye

     Vilevile Nnauye, alisema kama akizidi kukaidi amri ya Chama  cha CCM na Viongozi wa Mkoa wa Bukoba basi chama kitamfukuza uwanachama na Udiwani ambao anao ataukosa.

    Ikumbukwe, Januari 17, mwaka huu, Amani alikubali agizo la Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, baada ya CAG kuthibitisha kuwa miradi aliyokuwa akiitekeleza katika manispaa hiyo ilikiuka utaratibu na haikuwashirikisha madiwani.

     Mbali na Amani, wengine waliowajibishwa kwa kuvuliwa madaraka ni pamoja na aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Hamis Kaputa, aliyekuwa amehamia Mbeya, Mhandisi wa Halmashauri, Steven Nzihirwa na Mhasibu, Hamdun Ulomy.

No comments: