Tuesday, April 15, 2014

BUNGENI LEO--HIZI NDIZO KAULI ZA MBUNGE JOSEPH MBILINYI(SUGU) ALIYOYASEMA KUHUSU MBUNGE MWENZAKE MWIGULU NCHEMBA

    "Mwigulu Nchemba anataka Serikali moja, lakini anaogopa kusema"........... "Mhe.Mwenyekiti, kwanza naunga mkono Serikali tatu kama zilivyoletwa kwetu na TUME ya Katiba ya Jaji Warioba, kwa hiyo tunaunga mkono maoni Wananchi. Aliyeuharibu huu mchakato ni RAIS aliyekuja kueleza msimamo wa Chama chake badala ya kuzindua Bunge. Hiki ni Kipindi cha Kwaresma, acheni unafiki, tumeharibu Pesa nyingi. 

          CCM wameishiwa hoja, wameanzisha mkakati wa kuzomea. MWIGU...LU anataka Serikali moja, lakini anaogopa kusema. Tupo kwenye nafasi nzuri sana ya kulijadili Swala hili, la sivyo, tutalijadili kwa kulazimishwa. Leo LUKUVI anatutishia uwepo wa Serikali tatu, JESHI litaitawala Nchi! Mbona Rais wetu alikuwa Mwanajeshi na anatuongoza?...Wanajeshi ni Ndugu zetu, wakitawala kuna tatizo gani?... 
      
          Unapopimwa Malaria au Ukimwi, Sample ya Damu inatolewa kidoleni, na sio lita tano ili kujua ngoma imekaaje mwilini! acheni kutuzingua kwamba waliohojiwa na TUME ya Warioba ni wachache". amesema Mhe.Sugu.

No comments: