Monday, April 28, 2014

EXCLUSIVE---MANENO MAGUMU ALIYOYAZUNGUMZA ISMAIL RAGE LEO KUHUSU CHADEMA NA UKAWA.SOMA HAPA




        
 Na Karoli Vinsent    
   
MBUNGE Wa Tabora Mjini,Ismahil Aden Rage ametoboa Siri ya Kufanya Vibaya kwa Chama cha Demokrasia na Maendereo CHADEMA katika Chaguzi  mbalimbali hapa nchini,na kusema chama hicho kingojee Miujiza ili Kiweze Kushika Dola.
          
       Rage,aliyasema leo Jijini Dar es Salaam,alipokuwa anaongea na Mwandishi wa Mtandao huu na kusema kwa sasa Chama hicho kimepoteza mvuto kutokana na kuendeleza Siasa za Majitaka na kujuana kutoka kwa Viongozi wajuu wa Chama hicho,kutokana na kitendo cha chama hicho kumvua Uongozi na Uanachama Naibu Katibu Mkuu Bara Zitto Kabwe.

           “Kiukweli acha niseme Ukweli,Chadema kimepoteza Mvuto sana hususani kwa Vijana kutokana na Kitendo chake cha kumuondoa Zitto Kabwe,na ukweli ni kwamba huyu mtu anapendwa sana na Vijana sana mpaka ikafikia hatua hata sisi viongozi wa Chama Tawala tulikuwa tunapata Tabu sana,”


         “Leo Mwenyewe ni shuhuda Baada ya chama hicho kumvua Zitto Kabwe, uongozi pamoja na Uanachama tayari CCM,imeanza kupata ushindi kwenye Majimbo mbalimbali.Na hata mvuto wa chama hicho kwa Wananchi umeanza kupotea kuliko mwananzo,”alisema Rage.

       Rage,ambae pia ni Mjumbe wa Maalum la Katiba,katika hatua nyingine aliwataka Wajumbe wenzake wa Bunge la katiba kutoka UKAWA.warudi ili waendelee kutengeneza katiba ya Wananchi,kwani kufanya hivyo akukubaliki na Muungwana hana Budi kusamehe.

     Rage,vilevile ni Mwenyekiti wa Klabu ya Mpira wa Miguu ya Simba,alizidi kuongeza kwamba Rais Kikwete amefanya Jambo jema sana kuanzisha mchakato huu wa kupata  katiba mpya,kitendo cha UKAWA kufanya hivyo kutaifanya mchakato huo wa katiba kutofanikiwa na kupelekea pesa za walipa kodi kupotea kodi bule

No comments: