Tuesday, April 15, 2014

HABARI---KONGAMANO KUBWA LA MASWLA YA FILAMU LINAKUJA TANZANIA,SOMA HAPA

SELEMAN  WONDO AMBAYE NI CREATIVE DIRECTOR WA CREATIVE BASE AKIMKABIDHI CHETI RASMI CHA UBALOZI WA KONGAMANO HILO MSANII MAARIFU WA SANAA YA FILAMU TANZANIA PASTOR MIAMBA KATIKA UKUMBI WA HABARI MAELEZO

                   
                     Creativr Base Company ltd kupitia Kurugenzi yake ya Sanaa na Burudani kwa ujumla imeandaa kongamano la kitaifa (National Film Summit 2014, NFS 2014)ambalo litafanyika mwezi June 2014 hapa Dar es Salaam katika ukumbi wa Ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)jengo la Mawasiliano Tower, Ubungo.

                 Lengo la kongamano hilo ni kuunga mkono juhudi za Serikali kuitambua tasnia za filamu, kujadili changamoto zilizopo katika mfumo mpya wa uwekaji wa stamp za kodi katika kazi za fIlamu na muziki na namna ya kukabiliana nazo, kujadili changamoto za uzalishaji wa kazi bora za filamu na masoko yake,Hakimiliki na hakishiriki za kazi za Wasanii pamoja na umuhimu wa sera na sheria mbalimbali katika kusimamia tasnia ya Filamu Tanzania kwa Maslahi ya Taifa na kukuza pato la Wasanii nchini, Kutafuta ufumbuzi wa kudumu katika kuondoa tatizo la wizi wa kazi za Wasanii Tanzania,kuanzishwa mawanda ya ushirikiano na Wasanii wengine wan chi za Africa Mashariki na Kati.

               Kutokana na umuhimu wa tasnia ya filamu Tanzania, kamati ya Maandalizi ya .N.F.S ilikuwa na mchakato wa kutafuta balozi wa N.F.S 2014, kutokana na mchakato huo jumla ya Majina kumi na mbili ya Wasanii na waongozaji wa filamu Tanzania yalipendekezwa kuingia katika uteuzi wa Balozi wa National Film Summit 2014.

            Kutokana majina hayo kamati ya maandalizi ya N.F.S 2014 imemteua Ndugu Emanuel Myamba (Mkurugenzi wa Chuo cha Filamu Tanzania cha TFTC) kuwa Balozi wa National Film Summit 2014 – 2015.
           Mtaweza kujiuliza kwa nini kamati imemteua Emanuel Myamba kuwa Balozi wa National Film Summit 2014, Wasanii waliopendekezwa wana viwango sawa katika kazi zao lakini kuna cha ziada amabacho Balozi anatakiewa kuwa nacho ili kuonesha tofauti na washindani wengine,Kamati imemteua Emanuel Myamba kwa sababu pamoja na kuwa msanii mwenye mafanikio katika kazi za uongozaji na uchezaji wa filamu pia ameweza kuwa na kuwa na kituo mafunzo yakozi za tasnia ya filamu jambo ambalo ni muhimu kwa maendeleo ya Wasanii kuwa na Elimu, hivyo amewewezakuisaidia Serikali katika kukuiZa weledi wa Wasanii wachanga walio wakongwe kielimu.



No comments: