Tuesday, May 20, 2014

AZAMTV YAJA NA KWETU HOUSE (search for the Ultimate Fun)


Mkurugenzi mtendaji wa AzamTV, bwana Rhys Torrington
       AzamTV leo wamezindua mashindano yatakayowahusisha wapenzi wa kandanda yatakayojulikana kama KWETU HOUSE.  Mashindano haya  ambayo ni mara ya kwanza Tanzania yatashirikisha wapenzi na mashabiki wa mpira wa miguu ambapo  watu kumi wa 10 wa timu mbalimbali watachaguliwa na kuishi katika nyumba moja kwa muda wa siku 30 wakionyesha ni jinsi gani wao ni mashabiki namba mmoja kwa timu zao .     

      Akizindua mashindano hayo, Mkurugenzi mtendaji wa AzamTV, bwana Rhys Torrington alisema: Lengo kuu la kufanya shindano hili ni kuamsha hisia za mashabiki wa soka na kuonyesha umuhimu wa kuthamini mashabiki kwa sababu bila wao mpira wa miguu usingekuwepo leo hii; wakati huo huo ni kuwaletea watazamaji vipindi vinavyoburudisha na kuelimisha.
          
         Mashindano haya yametokana na ubunifu wa wafanyakazi wa Azamtv ambapo hiki ni kipindi kimojawapo kitakachofuatiwa na vingine vingi ambavyo viko ndani ya maandalizi kupitia kampuni ya Uhai Production ambayo ni kampuni mama ya AzamTV; aliongeza bwana Wasiwasi Mwabulambo ambaye ni mratibu wa mashindano hayo.

Mratibu wa shindano hilo wasiwasi mwabulambo akizindua rasmi
         Wanaoruhusiwa kushiriki mashindano haya ni wanaume wenye umri wa miaka kumi na nane (18) na kuendelea.

       Wakiwa ndani ya jumba la KWETU HOUSE washiriki wataenguliwa kila siku ya jumapili mpaka kubakia washiriki watatu ambapo mmoja wao atajinyakulia kitita cha shilingi milioni kumi (10)

     Usaili wa shindano hili utafanyika siku ya jumamosi  tarehe 24/05/2014 uwanja wa  Leaders club, kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 11 jioni. Usaili utakuwa ni bure.
Pia mashabiki wanaweza kujisajili kwa kutuma video zao fupi kwenda kwenye whatsApp number 0759 38 65 68 nakuonyesha ushabiki wao wa dhati.
Watakaochaguliwa watatangazwa tarehe 27/05/2014 ambapo wataingia ndani ya jumba la KWETU HOUSE tarehe 30/05/2014; na mshindi atapatikana tarehe 27/06/2014.

     Shindano hili limedhaminiwa na Azam Energy Drink kwa ushirikiano wa Channel Ten, Magic Fm na Times Fm.

No comments: