Tuesday, May 20, 2014

HABARI INAYOTIKISA JIJI KWA SASA----JESHI LA POLISI KANDA MAALUM DAR ES SALAAM LAANZA UCHUNGUZI WA KINA KUHUSU SABABU ZA KIFO CHA AFISA WA EWURA NDUGU JULIUS NITANGA GASHAZA


Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limeanza kufanya uchunguzi wa kina kuhusu sababu za kifo cha bwana JULIUS  S/O NITANGA @ GASHAZA , miaka 51, Meneja Biashara wa EWURA, Mkazi wa YOMBO VITUKA (Jet- Rumo). Afisa huyo alikutwa amefariki tarehe 18/05/2014, Kata ya YOMBO VITUKA, (M) Ilala katika nyumba ya kulala wageni iitwayo MWANGA LODGE katika chumba Na: 133 katika hali ambayo inaashiria kujinyonga kwa kutumia tai aliyokuwa ameivaa mwenyewe.

        Licha ya maelezo hayo, Jeshi la Polisi Kanda Maalum linafanya uchunguzi ili kuondoa utata ulioanza kujitokeza kuhusu kifo hicho hasa baada ya tarifa kuanza kuzagaa  kwamba kifo chake kilitokana na kutoelewana na viongozi wenzake katika masuala ya kikazi. Kinachofanyika ni kupata maelezo ya kina kuhusu mwenendo wa shughuli za marehemu na hali iliyomsibu kabla ya kifo chake kwani marehemu hakuacha ujumbe wowote aidha wa maandishi au wa mdomo.

        Aidha, Kamishna wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaa ameunda jopo la wapelelezi likiongozwa na Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum D’Salaam akishirikiana na wataalam wa Maabara Kuu ya Polisi (Forensic Bureau) katika kufanya uchunguzi wa kina kuhusiana na tukio hilo. Aidha maelezo mbali mbali ya mashahidi yanaendelea kuchukuliwa ili kujua kama kuna kosa la kijinai, kiutawala au yote.   

      Taarifa kamili ya mwelekeo wa shauri hili itatolewa hivi karibuni.

MAJAMBAZI WAWILI WALIOKUWA WANATAFUTWA WAKAMATWA WAKIMILIKI BASTOLA.

STORY NYINGINE KALI TOKA KWA KAMISHNA KOVA BOFYA CHINI


           
       Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata majambazi wawili huko KIWALANI MINAZI MIREFU, (M) Ilala wakiwa na Bastola moja aina ya STAR LANCER yenye namba SA CAL 22LR HK 708022 ikiwa na risasi moja ndani ya Magazine. Walipohojiwa walikiri kuhusika katika matukio kadhaa ya ujambazi na waliwataja wenzao ambao wamekuwa wakishirikiana nao katika matukio mbalimbali.
Majambazi hao waliokamatwa na silaha ni
·     
           ALLY S/O JUMA ALLY @ LIKWALE
·       CHARLES S/O CHIGANGA MALIMA @ PASTOR, miaka 32, mkazi wa 
    Tandale Uzuri.
Aidha, watuhumiwa waliotajwa kushirikiana na watuhumiwa hao wanasakwa kwa mbinu zote waweze kuwaonganisha na wenzao ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.


      KUKAMATWA NA MALI ISAFIRISHWAYO KWENDA NCHI JIRANI YA BURUNDIDRC PAMOJA NA WATUHUMIWA WATATU.

     Mnamo tarehe 18/05/2014 Jeshi la Polisi Kanda Maalum lilipokea taarifa  kutoka kwa msiri kuwa kuna gari lenye Na. T.649 BAY mali ya RUOTA INVESTIMENT limepakia mali iliyokuwa inasafirishwa kwenda nchini BUJUMBURA-BURUNDI kutoka kiwanda cha MURZAH OIL kwamba mali hiyo inashushwa huko Sinza Afrika Sana.

  Polisi walichukua hatua za haraka na kufika eneo la tukio na kukuta mali hiyo inashushwa kutoka katika lori hilo na kupakiwa kwenye gari namba T.571 APH aina ya Honda kwa ajili ya kubeba mzigo huo wa sabuni za unga aina ya Pulf na T-issue.

     Walipohojiwa wahusika kama mwenye mali ana taarifa juu ya kushushwa kwa mali hiyo walishindwa kutoa maelezo yanayoeleweka. Taratibu za kisheria zilifuatwa na watuhumiwa watatu wamekamatwa kwenye eneo la tukio ambapo walimtaja mtu mmoja aitwaye TAIRO S/O? kuhusika na tuhuma za mizigo hiyo.

    Inasemekana mali hiyo ina thamani ya Tshs 70,000,000/= (Shilingi Millioni Sabini) za kitanzania ambapo mali yote imeokolewa na Polisi inamtafuta mmiliki wa mali hiyo ili kuungana nae kukamilisha upelelezi wa shauri hilo.

  Watuhumiwa waliokamatwa kuhusiana na tukio hili ni
·       MWARABU S/O HAKIKA, Miaka 23, Mfanyabiashara, Mkazi wa kijitonyama.
·       IDD S/O JASINA, Miaka 48, Mfanyabiashara, Mkazi wa Kijitonyama.
·       RASHIDI S/O SAID, Miaka 17, Mkazi wa Kijitonyama.

                  KUKAMATWA KWA MAGARI SITA YA WIZI
         
        Mnamo tarehe 05/05/2014, Kikosi Maalum cha Kuzuia  na Kupambana na wizi wa magari kiliendesha oparesheni maalum katika jiji la Mwanza kwa kushirikiana na kikosi kazi cha Polisi Mwanza kuyatafuta magari kadhaa yaliyoibwa jijini Dar es Salaam katika matukio tofauti na siku tofauti. Hii ni baada ya Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam kupokea taarifa toka kwa wasamalia wema kisha kutuma kikosi hicho kwenda jijini Mwanza.

     Katika oparesheni hiyo yalipatikana magari sita aina mbamlimbali kama ifuatavyo:
·       
      Tarehe 06/05/2014, huko maeneo ya Nyakato Buzuruga ilikamatwa gari namba T.154 CRH, T/Mark II “Grande”, rangi “Pearl White” ikiendeshwa na  GEOFREY S/O ISAKA CHABA, Miaka 45, Mfanyabiashara, Mkazi wa Nyamanoro jijini Mwanza, aliyedai kuuziwa gari hilo na dalali YUSUFU S/O CHACHA, mkazi wa Mwanza. Gari hili inasemekana ni mali ya AIDA D/O AUGUSTINO HAULE, Miaka 35,  Mfanyabiashara, Mkazi wa Yombo Vituka jijini Dar es Salaam.

·       Tarehe 07/05/2014, maeneo ya Nyakato jijini Mwanza, ilikamatwa gari namba T.438 CKP, T/VEROSA, rangi “Pearl White”, ikiendeshwa na SHABAN S/O SALUM MGONJA, Miaka 24, Mfanyabiashara, Mkazi wa Nyakato Sokoni aliyedai kuuziwa  gari hilo na Mchungaji YUSUPH S/O ERNEST BUJIKU wa Kanisa la PENTEKOSTAl BUZURUGA jijini Mwanza. Gari hili liibiwa Yombo Vituka nyumbani kwa REHEMA D/O SAIDI ILUNGA, miaka 30, Mfanyabiashara.

·       Tarehe 08/05/2014, maeneo ya CAPRIPOINT karibu na Hotel ya Tilapia ilikamatwa gari namba T.787 BRW, T/CARINA SI, rangi ya Silver ikiwa imetelekezwa baada ya dereva kuona msako umekuwa mkali sana. Upelelezi wa awali unaonyesha gari hili liibwa huko Kinondoni  ambalo mmiliki wake ni AMANI S/O ABDALLAH MLILAPI wa jijini Dar es Salaam.

·       Aidha, tarehe 11/05/2014, maeneo ya katikati ya Jiji la Mwanza ilikamatwa gari namba T.895 CTU, T/Cresta GX 100, rangi ya Silver, ikiendeshwa na GODWIN S/O SHARTIEL KWEKA, miaka 28, mkazi wa Nyakato jijini Mwanza. Alieleza kuuziwa gari hilo na FIDELIS S/O LAURENCE KIMBAGE, miaka 36, mkazi wa Nyakato – jijini Mwanza. Gari hili liibiwa maeneo ya Kinyerezi Bonyokwa nyumbani kwa  VICTOR S/O BENSON USUMA, miaka 29, mfanyabiashara.
·       Pia, tarehe 14/05/2014, huko Mkoani Geita kwenye machimbo ya madini ya GEITA GOLD MINE lilikamatwa gari namba T.891 BFF, T/NOAH, Rangi Nyeupe, ikiendeshwa na VENANCE S/O BUKUKU, miaka 30, mfanyabiashara. Gari hilo liibiwa huko YOMBO BUZA nyumbani kwa SALUM S/O MWISHEHE KULITA, miaka 32, Afisa wa Bank ya NMB Makao Makuu.

·       Tarehe 04/05/2014 huko Morogoro, lilikamatwa gari namba T.570 BZX, T/NOAH, rangi ya Silver, ikiendeshwa na HUSSEIN S/O ALFAN SAID @ MASOFA, miaka35, Mfanyabiashara, mkazi wa Morogoro. Alipohojiwa alidai kuuziwa gari hilo na dalali SIWAMBALI S/O SAID MOHAMED. Gari hilo ni mali ya MOHAMED S/O GHALIB MWARABU, miaka 42, mkazi wa Ilala.
KUKAMATWA KWA MALI YADHANIWAYO KUWA YA WIZI
Jeshi la Polisi Kanda Maalum D’Salaam huko maeneo ya Tabata Matumbi limefanikiwa kukamata magari mawili yenye Namba T.539 BEX aina ya Mitsubish Canter rangi ya blue ikiwa imebeba mabox 180 ya misumari, na T.377 CME Toyota Noah rangi nyeupe likiwa limebeba mabox 42 ya balbu mali idhaniwayo kuwa ya wizi pamoja na watuhumiwa 3.
Hii ni baada ya Polisi waliokuwa doria kuyatilia mashaka magari hayo.

       POLISI WAZIDISHA MAPAMBANO DHIDI YA KERO YA FOLENI JIJINI D’SALAAM
Jeshi la Polisi Kanda Maalum D’Salaam limeamua kutumia mbinu mbali mbali mbadala ili kupambana kikamilifu na kero ya foleni inayowakabili madereva wa magari au vyombo vya moto jijini D’Salaam.  Mbinu hizo za kukabiliana na foleni ni pamoja na kuongeza idadi kubwa zaidi ya askari wa Jeshi la Polisi ambao watatanda katika barabara Kuu zinazoingiza magari mengi katikati ya Jiji wakati wa asubuhi na hatimaye wakati wa jioni, magari hayo na kwa wakati mmoja kutoka katikati ya jiji.  Mtandao huo mkubwa wa askari wa doria utaanza kazi kuanzia saa 10 alfajiri hadi saa 5 usiku wakati msongamano huo wa magari unapokuwa umepungua.  Askari hawa wa Usalama Barabarani na wengine kutoka vikosi mbali mbali watafanya kazi katika mtindo wa kupokezana (shift) ili kuleta ufanisi na ubora wa kazi.  Mtindo huu utawabana watumiaji wa barabara wenye mtindo wa kutanua ambao watakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria papo kwa papo (notification fines) au kufikishwa mahakamani bila msamaha au visingizio vyovyote.
Aidha uwepo wa askari hao kwa wingi barabarani utapunguza makosa ya usalama yanayofanywa kwa makusudi na wenye magari aua pikipiki ambao wengine hawajali ishara za taa za usalama barabarani (traffic lights), uchomekeaji usiozingatia taratibu za kiusalama, mwendo kasi, kuongea na simu za mkononi wakati dereva akiendesha gari, kutofunga mikanda ya dereva au abiria.  Aidha zoezi hili litaenda sambamba na ukaguzi wa uzima wa magari, kutokuwa na bima, leseni ya barabara (Road Licence) na uchakavu wa gari au pikipiki kwa ujumla.  Sambamba na zoezi hili tunaomba madereva raia wema watakaogundua madereva wanaofanya makosa ya makusudi mbele, nyuma au pembeni watoe taarifa Polisi kwa namba zifuatazo:-
1.0732 -928728           -        USALAMA BARABARANI KANDA MAALUM
2.0713-224848 -         MKUU WA USALAMA BARABARANI KANDA MAALUM
3.0787 – 668306               AU 022-2138177 – KIKOSI CHA 999
NAMBA  ZINGINE NI ZA WAKUU WA USALAMA BARABARANI MIKOA YA:
4.0713 – 207090         -        KINONDONI
5.0655 – 678260         -        ILALA
6.0658 – 376477         -        TEMEKE
Tahadhari inachukuliwa kwamba zoezi hili lina lengo la kuboresha kazi za Polisi na kuleta huduma bora kwa watumiaji wote wa barabara na kuondoa adha kubwa ya foleni yenye kuleta madhara ya kiuchumi na kijamii.


S.H. KOVA
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM



No comments: