Monday, May 26, 2014

KAMISHNA KOVA AMLILIA MWANDISHI MZEE MAX,ATOA RAMBI RAMBI YAKE,WENGINE TUIGE KWAKE

Na Karoli VInsent

        JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,lamlilia Aliyekuwa Mwandishi na mpiga Picha wa Kituo cha Runinga cha Mlimani Mzee Maxmiliani,ambaye aliyefariki Gafla kwa Presha.

       Kilio hicho, kimetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamishna Suleiman Kova,wakati wa Mkutano na Waandishi Habari, Ambapo alisema wao kama Jeshi la Polisi wamesikitishwa na Kifo cha Mwandishi wa huyo Mkongwe wa Habari na Mpiga picha Nchini.

     “Sisi  Jeshi la polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Tumesikitishwa sana na Kifo cha Mzee wetu huyo Bwana Maxmiliani,kwani amekuwa akitoa Mchango mkubwa,kwetu Jeshi la Polisi hususani Kanda hii ya Dar es Salaam kwa kuhakikisha Taarifa zinafika kwa Wananchi kutoka kwetu kwa wakati Muhafaka,”


      “Kwani Jeshi la polisi limekuwa likifanya Kazi kwa ukaribu mkubwa na Wanahabari kwasababu wamekuwa wakitoa Mchango mkubwa katika kuhakikisha Tarifa zetu kwa Umma”Alisema Kova
Kamishna, Kova alizidi kusema kutokana na Kugushwa na Msiba huo ameamua Kutoa Pesa ya Rambirambi shiringi Laki Moja,
“ Kutokana na Kugushwa na msiba huu mimi Binafsi nimetoa Fedha Taslim shiringi Laki moja,natunajaribu kujadiliana na Kanda Maalum  tujue tutafanya Utaratibu Mwingine”Alizidi kusema Kova

        Kwa upande wake Waandishi Mbalimbali waliozungumza na Mwandishi wa Mtandao huu hawakusita kuonyesha kusikitishwa na Msiba huo,kati yao ni Mwandishi Mwandamizi  wa habari kutoka kituo Cha Runinga cha Chanel Ten Mzee Kibwana Dachi.

      Ambapo,alisema amesikitishwa sana Kifo cha Mwandishi huyo wa Mlimani Tv,kwani yeye amemjua Miaka mingi sana, kutokana akitoa mchango mkubwa katika Taaruma hii ya Habari

         “Kwanza ngoja niseme, mimi nimeanza kumjua mzee maxmiliani siku nyingi sana,kusema kweli tasnii hii ya Habari imepoteza mtu muhimu sana kutokana kwa kufanya kazi kwa umakini sana na vilevile kushirikiana na wenzake bila ugomvi wowote”alisema Kibwana Dachi.

       Kibwana Dachi,ambae ni Mchambuzi wa Masuala Mbalimbali ndani Nchi na nje,aliwataka vijana wanaochipukia katika taaruma hii,kuiga mfano wa Mzee Maxmilian ili waweze kupata Mafanikio.

         Naye,Msomi wa Masuala ya Habari kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na vilevile ni Mwandishi Gazeti la Tanzania Daima,mwandishi John Magigi.alisema Taaluma ya Habari Nchini Imepoteza mtua Makini na mwenye Moyo wa Kujituma. 


No comments: