Thursday, May 15, 2014

ZIARA YA KINANA MKOANI TABORA YAIBUA MENGI,JIONEE HAPA


1Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili katika shule ya sekondari ya Kiwele kata ya Kitunda wilayani Sikonge mkoa wa Tabora ambapo amekagua miradi mbalimbali ya nyumba ya walimu na maabara zinazojengwa katika shule hiyo, Kinana akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi pia amekagua majengo ya kituo cha afya cha Kitunda, katika ziara hiyo mganga mkuu wa kituo hicho Dk.Silvanus Kabutula amelalamikia kuchelew kwa ujenzi wa jengo la upasuaji na kujifungulia akina mama wajawazito jambo ambalo linasababisha matatizo makubwa kwa wakati wa kata hiyo na vijiji vya jirani ambavyo vinategemea huduma kutoka katika kituo hicho, Akitolea ufafanuzi zaidi kuhusu suala hilo mbunge wa jimbo la Sikonge Mh. Said Mkumba amesema, mkandarasi wa ujenzi wa vituo hivyo ameshindwa kumaliza kazi kwa wakati na mkataba ulianza 28/ 10/2009 na ulitakiwa kumalizika 2/5/2011 lakini mpaka sasa vituo hivyo na zahanati havijakamilika jambo ambalo linakwamisha ustawi wa jamii katika suala zima la afya, Ameongeza kuwa kupitia mradi wa Mradi wa kupunguza vifo kwa akina mama Support to Martenal Mortality Project Reduction (SMMRP)  jumla ya vituo saba vya kutolea huduma wilayani Sikonge vilitakiwa kujengwa ambavyo ni Kipili,Kitumbi,Tumbili, Pangale,Kitunda, Mazinge na Kisanga ambapo jumla ya shilingi  bilioni 2,051,723,850 zimelipwa kwa mkandarasi huyo hata hivyo kazi hiyo jaijakamilika mpaka sasa, Kuhusu za la Tumbaku Mkumba amesema wakulima wa tumbaku waruhusiwe kuuza tumbaku wanapotaka kwa sababu vyama vya ushirika vya msingi vinawadhulumu wakulima hao. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ameahidi kufikisha kwa suala hilo kwa Mh. Rais Dr. Jakaya Mrisho Kikwete kilio cha wananchi wa Sikonge kuhusu suala la zahanati hizo  kutokumalizika kwa wakati na matatizo ya wakulima kutolipwa fedha zao za mauzo ya tumbaku kwa wakati.(PICHA NA  FULLSHANGwe
2Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi akiwasili katika shule hiyo. 3Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua moja ya nyumba za walimu katika shule ya sekondari ya kiwele Kitunda. 4Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akisaini kitabi  wakati alipowasili katika kituo cha afya cha Kitunda, Kushoto ni Mganga mfawidhi wa kitu hicho Dk. Silvanus Kabutula. 5Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akiaikiliza taarifa ya mganga mfawidhiwa kituo cha afya cha Kitunda Dk. Silvanus Katubula 6Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua kituo cha afya cha Kitunda huku akongozana na Mh. Said Mkumba mbunge wa jimbo la Sikonge. 7Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na mganga mfawidhi wa kituo cha afya cha Kitunda wakati akikagua miradi ya maendeleo katika kituo hicho, kulia ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi Siasa na Uenezi. 8Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akimsiiliza mganga mfawidhi wa kituo cha afya cha Kitunda Sikonge wakati alipotembelea kituo hicho kutoka kulia ni Mh. Said Mkumba mbunge wa jimbo la Sikonge na anayefuata ni Nape Nnauye. 9Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili katika eneo la mkutano wa hadhara kata ya Kitunda. 10Kwaya ikitumbuiza katika mkutano huo. 11Kikundi cha ngoma kikitumbuiza katika mkutano huo. 12Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi. Fatma Mwassa akimueleza jambo Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana wakati wa mkutano huo , kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi na aliyesimama nyuma ni mbunge wa jimbo la Sikonge Mh. Said Mkumba. 13Kikundi cha kwaya ya Kitunda kikitumbuiza katika mkutano wa hadhara. 14Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi. Fatma Mwassa akizungumza na wananchi wa kata ya Kitunda kuhusu zao la Tumbaku 15Mbunge wa jimbo la Sikonge Mh. Said Mkumba akizungumza na wananchi wa kata ya Kitunda 16Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi  akizungumza na wananchi wa kata ya Kitunda katika mkutano wa hadhara. 17Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutunia wananchi wa kata ya Kitunda. 18Juma Bakari Kaseka Mkulima wa tumbaku kata ya Kitunda wilayani Sikonge akizungumza katika mkutano wa hadhara na kutoa malalamiko ya wakulia kwa jinsi wanavyoibiwa fedha zao za mauzo ya Tumbaku. 19Bw. Lameck Mnyama mkulima na  Mjumbe wa mkutano mkuu wa Chama Kikuu cha Ushirika wa wakulima wa tumbaku (WETCO)akilalamikia jinsi wakulima wanavyodhulumiwa  huku akionekana kuchoka kabisa wakati  akielezea wizi unaoendelea kwa wakulima wa tumbaku wakati wa malipo ya mauzo ya tumbaku yao jambo ambalo linapoteza imani yake kwa chama hicho pamoja na kwamba yeye ni mmoja wa viongozi wa (WETCO)

No comments: