Friday, August 29, 2014

LIVE TOKA DAR--MANJI ACHARUKA SAKATA LA OKWI,SOMA KAULI ZAKE NZITO LEO

Na Karoli Vinsent
    KUFUATIA mchezaji Emmanuel Okwi kuikacha klabu ya Yanga na kujiunga kwa wapinzania wa Jadi wa timu hiyo, Klabu ya Simba.

     Mwenyekiti wa Klabu Yanga Yusuph Manji ameibuka na kuwataka wanachama pamoja na Mashabiki wa Yanga kuwa wapole katika kipindi hiki,na Badala yake Yanga wamesema wanataka Fidia kutoka kwa Mchezaji huyo pesa za kimarekani dola laki tano, sawa na pesa za Kitanzania zaidi ya milioni 700 kwa kitendo chake cha kuvunja sheria za mpira wa miguu nchini.
            
         Hayo yamesemwa mda huu Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Yanga,Yusuph Manji wakati wa Mkutano na Waandishi  wa Habari kuzungumzia suala nzima la usajili,ambapo Manji amesema klabu hiyo haina ugomvi na Simba kwani wameshirikiana sana kwenye mambo mengi  ila  anashangaa rafu mbaya iliyofanyiwa klabu hiyo,wakati wa kumsajili Emmanuel Okwi.

      
     “Kiukweli Klabu ya Simba ni marafiki zetu sana ila nashangaa  jinsi walivyotufanyia kwenye usajili wa mchezaji Emmanuel Okwi maana ni rafu,kwasababu ukisoma sheria ya mpira wa miguu ya FIFA namba 17 kigungu cha tano kinasema wazi kuhusu usajili ni kwamba klabu yeyote inaotaka kumsajili mchezaji wa timu nyingine inapaswa kuwasiliana na Timu husika,lakini wenzetu Simba hawajawasiliana na sisi,kutokana na hujuma hii yanga tunataka fidia za dola laki tano sawa na pesa za Kitanzania zaidi ya milioni 700 ”alisema Manji.

      Manji alizidi kusema Klabu ya Yanga tayari imeliandikia barua shirikisho la Soka nchini TFF na kuwapa siku saba wawe wametoa hukumu kwa Simba ikiwemo kulipwa fidia hiyo,
Aidha Manji alisema Klabu hiyo haisikitiki kwa kuondoka kwa mchezaji huyo kwani wachezaji wengi waliokuwapo Klabuni hapo na wameondoka ila wao wanasikitika kwa kuvunjwa Sheria .

      “Mimi nashangaa sana watu wanavyosema Yanga inametuhuma sana kuondoka kwa Okwi,ila jibu ni hapana kwani hapa Yanga wameondoka wakina Kavumbagu,Domayo wamekwenda klabu ya Azam mbona hatujasikitika?kwanza Okwi ni mchezaji wa Kawaida sana naweza kusema  katika mechi 13 za ligi alizocheza Yanga msimu uliopita katika mechi sita kashinda goli moja tu sasa tumsikitike nin?”alisema Manji.
  
      Vilevile mwenyekiti huyo aliwataka Wanachama pamoja na wapenzi wa Yanga nchini kuwa wapole na kuuwaachia uongozi wa Yanga unavyolishughulikia suala hilo.
   
      Habari za Mchezaji huyo wa Kimataifa kutoka Uganda Emmanuel Okwi kuihama klabu hiyo zilizopatikana jana jioni, zilisema nyota huyo ambaye hatima yake ndani ya klabu ya Yanga ilikuwa gumzo kubwa, jana alitarajiwa kusaini mkakaba huo kuwatumikia Wekundu wa Msimbazi kwa kipindi kingine.
  
         Kurejea kwa Okwi Msimbazi, kunamweka katika wakati mgumu mchezaji Benard Musoti, nyota wa kimataifa wa Kenya, kwani sasa ni yeye  anayechungulia dirisha la kutokea, ama Pierre Kwizera.
         
    Okwi kutua Simba, ni kama kurejea nyumbani kwani ndio klabu aliyojiunga nayo kwa mara ya kwanza nchini akitokea Uganda na kung’ara nayo, kabla ya kuihama na kujiunga Etoile du Sahel ya Tunisia na kisha Yanga.
         
      Sheria za usajili za Ligi Kuu Tanzania Bara zinataka klabu kuwa na nyota wa kigeni wasiozidi watano na mbali ya Okwi, nyota wengine wa kimataifa katika kikosi cha Simba ni, Raphael Kiongera, Joseph Owino, Musoti, Kwizera na Amisi Tambwe.
         
      Mapema jana kabla ya Okwi kutua Simba, benchi la timu ya Simba, lilisema bado linamuhitaji Donald Musoti na kudokeza kuwa, haliridhishwi na kiwango cha Hussein Butoyi.
          
      Butoyi, nyota wa kimataifa wa Burundi aliyetua Simba, hivi karibuni kuziba nafasi ya Musoti aliyekuwa mbioni kutemwa, lakini akishindikana kutokana na ugumu wa mkataba wa nyota huyo.
            
      Musoti, ambaye miongoni mwa nyota Simba waliofanya vema msimu uliopita, amebakiza mkataba wa mwaka mmoja na nusu.
           
     Habari zilizopatikana jana kuutoka ndani ya Simba, zilisema, baadhi ya viongozi walimuhitaji Butoyi na wengine wakisapoti hatua ya benchi la ufundi kumtaka Musoti kutokana na kiwango chake.
         
      “Benchi la ufundi, linamuhitaji Musoti aendelee kukipiga Simba, hata mimi binafsi, Musoti namuona anafaa, huyo Butoyi hamna kitu kabisa, wanaosema wanalingana uwezo sio kweli, Musoti anajua bwana,” kilisema chanzo hicho.



No comments: