Mwenyakiti wa CHADEMA taifa MH FREMAN MBOWE akiwasili ukumbi wa mliman city kwa ajili ya kuzungumza na wamama wa chama hicho mapema leo |
Mwenyekiti wa chama cha demcrasia na maendeleo (chadema)
taifa mh FREMAN MBOWE amesema kamwe wanawake wa chama hicho wasitarajie kupewa
nafasi za upendeleo katika uongozi wa chama hicho kwani chama chake hakipo kwa
ajili ya kugawa zawadi ya vyeo na badala yake wajitume kuhakikisha wanakuwa na
uwezo unaotakiwa katika kuongoza chama hicho.
Kauli hiyo ameitoa muda huu jijini Dar es salaam
wakati akizungumza na wanawake wa chama hicho nchi nzima wakati akifungua
mkutano wa baraza la wanawake la chadema BAWACHA mkutano ambao utaitimishwa kwa
kupatikana viongozi wapya wa chama hicho.
MH MBIOWE ambapo muada mwingi ameonekana kuwasihi wanawake kuacha majungu ndani kwa ndani na badala yake wafanye kazi ya kujenga chama hicho kwa lengo la kuchukua dola mwakani |
Mh MBOWE amesema kuwa hakuna kubebana katika maswala muhimu kama uongozi kwani
chadema ni chama makini na ni lazima kuhakikishe kuwa kinakuwa na viongozi
makini na wenye uwezo wa kuleta mabadiliko ndani ya nchi hivyo hakitakuwa na
msamaha wowote kwa mwanamke ambaye atadhani kuwa anastahili kupewa uongozi hata
kama hana sifa za kuwa kiongozi.
“ndugu zangu wanawake naomba muelewe jambo
moja,pamoja na kuwa tunatakiwa kuhakikisha kuwa wanawake wanawezeshwa ili wawe
na haki sawa na wanaume lakini hatuwezi kutenda dhambi ya kumpa mtu cheo hata
kama hana sifa eti kwa sababu ni mwanamke,hatutoi zawadi ya vyeo ndani ya chama
chetu,tunahitaji wanawake majasiri,wenye moyo wa kuwakomboa watanzania,hivyo
kama umegombea nafasi yoyote katika chama hichi ukidhani kuwa tutakubeba kwa
kuwa wewe ni mwanamke mimi nasema hatuko tayari”amesma mbowe.
Akizungumzia mchakato wa katiba mpya na ulipofikia
mh MBOWE amesema kuwa wao kama UKAWA sasa wamechoka na michezo wa kitoto ambao
amesema unachezwa na baadhi ya viongozi wa ccm juu ya mchakato huu hivyo sasa
wameamua kufanya jambo tofauti ambapo amesema kuwa jumapili ijayo umoja wao
wameamua kukutana na watanzania wote kwa wakati mmoja na kuwaeleza ukweli wote
wa kwanini mchakato huo umekwama ambapo hakutaja njia ambayo wataitimia
kukutana na watanzania wote kwa wakati mmoja.
Mbunge wa ubunge MH JOHN MNYIKA naye alikuwepo katika mkutano huo |
Wanawake kutoka kila kona ta TANZANIA wakicheza kwa furaha muziki kabla ua kuanza kwa shughuli hiyo rasmi |
Hapa lilitumika neno moja tu pipoooooooooooooooooo------ |
“naomba
nisema machache juu ya mchakato wa katiba,unajua kuna mchezo mchafu sana
tunachezewa ila mi nasema ni wakitoto sana,sisi kama ukawa tumeamua kuwaeleza
watanzania wote mwenendo wa mchakato mzima siku ya jumapili na naomba wanawake
mttunge mkono”
Aidha amesema kuwa katiba mpya lazima ipatikane hata
miaka mia ijayo itapatikana tu ila cha msingi ni kupata katiba itakayowasaidia
watanzania wote na sio kuwasaidia wachache kama ilivyo sasa.
Baraza la wanawake la chadema BAVICHA linaingia
katika mchakato wake wa kuwapata viongozi wapya ikiwa ni baada ya hapo jana baraza la
vijana BAVICHA kufanya uchaguzi wao ambapo bw PASTROBAS PASCAL aliibuka mshindi wa nafasi
ya uenyekiti akichukua mikoba ya JOHN HECHE aliyemaliza muda wake.
Mamia ya wanawake wa chama hicho wakiwa wanasikiliza kwa makini katika mkutano huo ambao unaendele hapa mlimani city jijini Dar es salaam |
No comments:
Post a Comment