Kamishna KOVA akiwa katika mkutano huo |
Kamishna wa Polisi Kanda Maalum Dar es salaam Suleiman Kova amewataka askari wote wa Kanda hiyo kufanyakazi kwa weledi, kuzingatia haki za binadamu, na kufuata maadili ya kazi katika utendaji wao wa kila siku.
Kamishna Kova ameyasema hayo wakati akiongea na Maafisa na Wakaguzi katika kikao cha utendaji kilichofanyika katika ukumbi wa Bwalo la Maafisa Oysterbay, Kinondoni, jijini Dar es Salaam na kusisitiza umuhimu wakutoa huduma bora kwa wateja kulingana na matarajio ya wananchi.
Aidha Kamishna Kova amesisitiza usiri katika Taarifa zinazoletwa /zinazotolewa na wananchi na kwamba kwa kufanya hivyo kutalifanya Jeshi la Polisi kuaminika kwa wananchi. Akizungumzia suara la rushwa, Kamishina Kova amewaasa askari kutojihusiasha na kupokea rushwa kwani ni adui wa haki na kinyume na maadili ya kazi za Polisi.
Amehimiza ushirikishwaji wa wananchi katika kila hatua hasa katika mashauri mbalimbali ya kesi zao na kutenda kazi kwa uwazi hasa wakati wananchi wanapotakiwa kupata taarifa za mashauri yao au wanapoomba ushauri katika kero zinazowasibu.
Kila Afisa, Mkaguzi na askari lazima afanye kazi kwa bidii na ukakamavu ili mchango wa Jeshi la Polisi uonekane wazi kwa jamii ya watanzania na wageni wanaoingia na kutoka nchini pia wale wanaoishi nchini.
No comments:
Post a Comment