Monday, October 6, 2014

HABARI NJEMA LEO KUTOKA WIZARA YA MAWASILIANO SAYANSI NA TECHNOLOJIA.SOMA

Na karoli Vinsent

     SERIKALI nchini imesema ifikapo mwakani mwezi wa kumi Hospitali zote za Rufaa nchini zitaunganishwa kwenye mkongo wa Taifa kwa lengo la kuboresha huduma za afya nchini.
             
       Hayo yamesemwa leo Jijini Dar Es Salaam na Waziri wa Sayansi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati akizindua huduma mpya na ya kisasa ya Video ya mikutano,ambapo Profesa Mbarawa alisema Mkongo wa Taifa umekamilikia kwa asilimia kubwa na kuongeza ifikapo mwakani watahakikisha hospitali zote nchini zinaunganishwa kwenye mkongo wa taifa hili kuongeza ubunifu na uwajipikaji kwa watendaji wa Afya.
           
          Profesa Mbarawa alizidi kusema nia ya Wizara yake ni kuifanya Sekta ya “Internet”Mtandao Inakua kwa kasi hapa nchini na kuleta Tija katika  Taifa huku ikizingatia Dunia kote sekta ya Mawasiliano imekuwa muhimili wa uchumi.

       
       Vilevile Profesa Mbarawa alisema kwa kuzinduliwa kwa Huduma ya Video Mkutanoni itapunguza gharama ilizokuwa inazipata Serikali kwa kutenga Fedha kwa  Watendaji kusafiri kutoka mkoa mmoja hadi mkoa mwingine kwa ajili ya Kikao lakini kwa mfumo huu mpya uliozinduliwa leo utawaondolea Adha hiyo na kuwafanya watendaji wa mikoa na Wilaya kukaa walipo na kutumia njia ya Video kuwasiliana na watendaji wengine pasipo kwenda kwenye eneo la tukio.
               
      Aidha, Profesa Mbarawa aliwataka watanzania kutumia mitandao ya Kijamii kwa lengo ya kupata taarifa na kuongeza ujuzi wa mambo na kuacha tabia hasi ya kutumia mitandao ya Jamii kuchafua watu na kuonyesha picha chafu.

       Huduma ya Video ya Mkutanoni imeanza kwa Mikoa zaidi ya mitano ambapo huduma hiyo itapunguza urasimu uliopo wa kutumia Fedha nyingi za Serikali.



No comments: